Aya 83 – 99: Ibrahim Alikuwa Katika Kundi Lake
Lugha
Neno kundi limefasiriwa kutokana na neno la kiarabu shia’ lenye maana ya mfuasi anayefuta dini na njia ya yule anayemfuata. Kisha neno hili shia likazoeleka kuwa na maana ya mfuasi wa Imam Ali (a.s.) na yule aliyechukua nafasi yake katika watoto wake.
Maana
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake.
Kundi lake, yaani kundi la Nuh. Maana ni kuwa Ibrahim alifuata njia ya Nuh kiitikadi na kimatendo. Mfasiri mmoja wa kale anasema kuwa baina ya Nuh na Ibrahim kulikuwa na miaka 2640. mwenye kauli hii hakutege- meza kwenye rejea za kutegemewa.
Alipomjia Mola wake kwa moyo ulio salama.
Mwenye moyo huu ni yule aliyemfanyia ikhlasi Mwenyezi Mungu peke yake katika kauli zake na vitendo vyake vyote. Kuna Hadith isemyo: “Imani ya mja haisimami sawa mpaka usimame sawa moyo wake.” Kwenye Nahjul-balgha kuna maneno haya: “Heri zote ni za moyo ulio salama uliomtii anayeuongoza na kujiepusha na anayeudekeza.”
Alipomwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini? Je, kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
Ibrahim alipinga ibada ya masanamu kwa watu wake akawakabili na kauli ya haki kwa kusema kuwa mnataka uzushi na batili kwa kumrejea asiyekuwa Mwenyezi Mungu na kujikurubisha kwa ibada kwa asiyekuwa Yeye? Umetangulia mfano wake katika Juz.7 (6:74).
Mnamdhania nini Mola wa walimwengu wote?
Je, mnamdhania kuwa ni jiwe au nyota naye ameumba ulimwengu? Je, akili yenu haiamki hata kidogo au kuzinduka kutokana na ujinga huu?
Katika Juz. 13 (13:16), kifungu cha ‘akili za watu haziwatoshelezi,’ tumebinisha kwa nini washirikina waliabudu mawe yanayokojolewa na mambwa na vicheche?
Kisha akapiga jicho kutazama nyota, akiwapa dhana watu wake kuwa anatafuta muumba wa ulimwengu, kwa vile wao walikuwa wakiabudu miungu mingi; hasa Nanar, mungu wa mwezi na mkewe Nanjal; kama ilivyoelezwa katika Kamusi ya Kitabu kitakatifu.
Maana ya Aya hii yamekuja katika Juz. 7 (6:74-79).
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
Wafasiri wana kauli nyingi kuhusu makusudio ya ugonjwa. Yenye nguvu zaidi ni ile inayosema kuwa makusudio ya ugonjwa hapa ni shaka. Na maana yanakuwa kwamba Ibrahim aliwaambia watu wake, mimi hivi sasa nimedangana natafuta ukweli na uhakika ili niweze kuongoka kuweza kumjua muumbaji.
Nimeangalia masanamu nikapata uhakika kuwa hayawezi kuwa miungu; kisha nikaangalia nyota na sikupata mwongozo wowote; nimebaki kwenye shaka na kudangana.
Mfumo wa Aya unasaidia maana haya au angalau unayapa nguvu, kwa sababu yanaunganisha baina ya kuangalia kwenye nyota na kuwa mgonjwa.
Wala kauli yake hii ya kusema ana shaka hatuwezi kusema kuwa ni uwongo, kwa sababu ni katika hali ya kwenda na mbishani ili kumchukua kwenye hoja na kumkatia nyudhuru zote.
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
Walimwacha na wakajiendea zao.
Basi akaiendea miungu yao kwa siri.
Alichukua fursa ya kuondoka kwao na kwenda haraka kwenye masanamu. Walikuwa wameyawekea chakula ili yakibariki, akaiambia:
Mbona hamli? Mna nini hata hamsemi?
Alisema hivi kwa kuibeza na kutoa hoja kwa anayeiabudu na kutabaruku nayo.
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kuume.
Aliavunja masanamu vipande vipande kwa mkono wake wa kuume na kabakisha kubwa lao, angalau waweze kurejea.
Basi wakamjia upesi upesi.
Watu walikuja haraka kwa Ibrahim na kuanza kumuuliza: wewe ndiwe uliyeifanyia hivi miungu yetu?
Akasema: Je, mnaviabudu vitu mnavyo vichonga?
Yaani ole wenu! Msimzulie Mwenyezi Mungu uwongo. Hakika Mola ni Muumba sio muumbwa na Mwenye kuruzuku sio mwenye kuruzukiwa. Nyinyi mmeyatengeneza masanamu haya kwa mikono yenu na mnayalinda, vipi yatakuwa miungu?
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliyewaumba nyinyi na mnavyovifanya!
Yeye ndiye Muumba wa kila kitu na marejeo ni kwake.
Wakasema: Mjengeeni jengo, kisha mtupeni motoni.
Walishindwa kuikabili hoja kwa hoja, wakakimbila maguvu; kama ilivyo hali ya mataghuti, huwasha moto na kuwatupa humo wapigania haki na kheri; kama ilivyokuwa zamani. Na elimu ya uvunjaji ilipoondelea sasa wanautupa moto kwa wananchi wanyonge pamoja na wanawake na watoto wao.
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini, pale alipoufanya moto ni baridi na salama kwa Ibrahim.
Na akasema: Hakika mimi nakwenda kwa Mola wangu ndiye atakayeniongoza.
Baada ya Mwenyezi Mungu kumwokoa Ibrahim na vitimbi vya watu wake, alihama kutoka mji wake wa Urulkaldaniyya (Chaldeans) – Babilon – kwenda Sham.
Katika Kamusi ya Kitabu kitakatifu imeandikwa: “Yaligunduliwa mabaki na michoro ya mika elfu mbili kabla ya miladi (B.C.).
Lilikutwa jina la Ibrahim kwa mfumo wa Abramu au Abrama. Ugunduzi wa historia wa sasa umedhihirisha hali ya mji wa Uru, aliouhama Ibrahim, kama ulivyokuwa wakati huo.”
Umetangulia mfano wake kwa ufafunizi kidogo kwenye Juz. 17 (21:51-60).
رَبِّ هَبْ لِي مِنَ الصَّالِحِينَ {100}
فَبَشَّرْنَاهُ بِغُلَامٍ حَلِيمٍ {101}
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ السَّعْيَ قَالَ يَا بُنَيَّ إِنِّي أَرَىٰ فِي الْمَنَامِ أَنِّي أَذْبَحُكَ فَانْظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَا أَبَتِ افْعَلْ مَا تُؤْمَرُ ۖ سَتَجِدُنِي إِنْ شَاءَ اللَّهُ مِنَ الصَّابِرِينَ {102}
فَلَمَّا أَسْلَمَا وَتَلَّهُ لِلْجَبِينِ {103}
وَنَادَيْنَاهُ أَنْ يَا إِبْرَاهِيمُ {104}
قَدْ صَدَّقْتَ الرُّؤْيَا ۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ {105}
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْبَلَاءُ الْمُبِينُ {106}
وَفَدَيْنَاهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍ {107}
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ {108}
سَلَامٌ عَلَىٰ إِبْرَاهِيمَ {109}
كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ {110}
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ {111}
وَبَشَّرْنَاهُ بِإِسْحَاقَ نَبِيًّا مِنَ الصَّالِحِينَ {112}
وَبَارَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰ إِسْحَاقَ ۚ وَمِنْ ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌ وَظَالِمٌ لِنَفْسِهِ مُبِينٌ {113}