Aya 101 – 102: Miji Hiyo Tunakusimulia
Maana
Miji hiyo tunakusimulia baadhi ya habari zake.
Miji hiyo ni ishara ya watu wa miji hiyo ambao ni aina tano: Watu wa Nuh, wa Hud, wa Swaleh, wa Lut na wa Shuaib.
Maneno yanaelekezwa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, Nabii Muhammad (s.a.w.) wakikusudiwa waislamu kupewa habari ya hali za waliopita, ili wazingatie na watahadhari.
Hakika waliwajia Mitume wao kwa ishara zilizo waziwazi, lakini hawakuwa wenye kuamini waliyoyakadhibisha zamani.
Ametaja Razi njia tatu za kutafsiri kipande hiki cha Aya, na Tabrasi naye akazidisha ya nne. Hakuna hata moja waliyoitilia nguvu, na wakamwacha msomaji wa kawaida kwenye mataa; ambapo maana yako wazi yasiyokuwa na undani wowote.
Kwa ufupi ni kuwa watu wa miji hiyo kabla ya kupelekewa Mitume wa Mwenyezi Mungu, walikuwa kwenye shirki na upotevu; na kwamba wao waliendelea katika shirki yao na upotevu baada ya kuwafikia Mitume kwa dalili na miujiza. Na hawakuathirika na chochote, wakawa kama ambao hawakupelekewa mjumbe anayetoa bishara na maonyo. Haya yanafahamishwa na kauli yake Mwenyezi Mungu:
Namna hii Mwenyezi Mungu anazipiga muhuri nyoyo za makafiri.
Muhuri hapa ni fumbo la kususuwaa kwa nyoyo zao na kwamba hazijali kupotea kwake wala haitarajiwi kheri yake.
Na hatukuona kwa wengi wao ahadi yoyote.
Hawaamini dini ya Mwenyezi Mungu wala hawalazimiani na chochote kinachohusiana na ubinadamu. Hata hivyo wanayo ahadi moja tu wanayolazimiana nayo wala hawapingani nayo, nayo ni kufuata masilahi na hawaa.
Na hakika tuliwakuta wengi wao ni mafasiki.
Yaaniwamepoteakufuatanjia.
ثُمَّ بَعَثْنَا مِنْ بَعْدِهِمْ مُوسَىٰ بِآيَاتِنَا إِلَىٰ فِرْعَوْنَ وَمَلَئِهِ فَظَلَمُوا بِهَا ۖ فَانْظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُفْسِدِينَ {103}
وَقَالَ مُوسَىٰ يَا فِرْعَوْنُ إِنِّي رَسُولٌ مِنْ رَبِّ الْعَالَمِينَ {104}
حَقِيقٌ عَلَىٰ أَنْ لَا أَقُولَ عَلَى اللَّهِ إِلَّا الْحَقَّ ۚ قَدْ جِئْتُكُمْ بِبَيِّنَةٍ مِنْ رَبِّكُمْ فَأَرْسِلْ مَعِيَ بَنِي إِسْرَائِيلَ {105}
قَالَ إِنْ كُنْتَ جِئْتَ بِآيَةٍ فَأْتِ بِهَا إِنْ كُنْتَ مِنَ الصَّادِقِينَ {106}
فَأَلْقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعْبَانٌ مُبِينٌ {107}
وَنَزَعَ يَدَهُ فَإِذَا هِيَ بَيْضَاءُ لِلنَّاظِرِينَ {108}
قَالَ الْمَلَأُ مِنْ قَوْمِ فِرْعَوْنَ إِنَّ هَٰذَا لَسَاحِرٌ عَلِيمٌ {109}
يُرِيدُ أَنْ يُخْرِجَكُمْ مِنْ أَرْضِكُمْ ۖ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ {110}
قَالُوا أَرْجِهْ وَأَخَاهُ وَأَرْسِلْ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ {111}
يَأْتُوكَ بِكُلِّ سَاحِرٍ عَلِيمٍ {112}