Majlisi Ya 9: Imam Husein (a.s.) Aazimia Safari Ya Iraq
Imam Husein (a.s.) alipoazimia kwenda Iraq alisimama akatoa hotuba akasema: "Hamu yangu ya kukutana na wazazi na ndugu zangu waliotangulia (kufariki) ni kama shauku aliyokuwa nayo Yaaqub kwa mwanawe Yusuf (alipopotea) na kifo kitakchonifika kwangu ni jambo bora, kwani naona viungo vya mwili wangu vitakatwakatwa na maadui zangu hapo katika jangwa lililo baina ya Nawasiisi na Karbala.