Majlisi Ya 9: Imam Husein (a.s.) Aazimia Safari Ya Iraq

Imam Husein (a.s.) alipoazimia kwenda Iraq alisimama akatoa hotuba akasema: "Hamu yangu ya kukutana na wazazi na ndugu zangu waliotangulia (kufariki) ni kama shauku aliyokuwa nayo Yaaqub kwa mwanawe Yusuf (alipopotea) na kifo kitakchonifika kwangu ni jambo bora, kwani naona viungo vya mwili wangu vitakatwakatwa na maadui zangu hapo katika jangwa lililo baina ya Nawasiisi na Karbala.

Swahili

Majlisi Ya 8: Maafa Yaliyompata Muslim Bin Aqiil

Muslim Bin Aqiil zilipomfikia habari za matendo aliyoyatenda Ibn Ziyad kumtendea Hani, alitoka yeye pamoja na watu waliokuwa wakimtii kwenda kumsaidia Hani na kumuokoa, pia kupigana na Ibn Ziyad.

Ibn Ziyad alipogundua jambo hilo alijificha katika jumba hilo la utawala wa Bani Umayya, ikawa wafuasi wake ndiyo wanapigana na watu wa Muslim bin Aqiil.

Wafuasi wa ibn Ziyad waliokuwa pamoja naye wakawa wanachungulia na kuwatahadharisha wafuasi wa Muslim bin Aqiil na wakawaonya kuwa litakuja Jeshi kutoka Sham kwa Yazid nalo litawashambulia.

Swahili

Majlisi Ya 7: Yaliyotokea Al-Kufah Baada Ya Ibn Ziyad Kufika Hapo

Ibn Ziyad alipokwisha wasili katika mji wa AI-Kufah, alijiimarisha kwa kutawanya majasusi kufuatilia nyendo za Muslim bin Aqiil. Matokeo ya ujasusi huo yalimfanya yeye Ibn Ziyad afahamu kuwa Muslim bin Aqiil yuko katika nyumba ya Bwana Hani.

Kwa hiyo Ibn Ziyad aliwaita mabwana Muhammad bin al-Ashath na Hasan bin Asma bin Kharijah na Amru bin al-Hajaaj akawaambia, "Ni kitu gani kinamfanya Hani asije kwetu (kutusalimia)?"

Swahili

Majlisi Ya 6: Yaliyotokea Makka Baada Ya Imam Husein (a.s.) Kufika Hapo

Ilipofahamika kwa wakazi wa Makkah kwamba, Imam Husein (a.s) yupo Mjini hapo, wakazi wa Mji huo walianza kumtembelea kwa wingi.

Miongoni mwa watu waliofika kwake ni pamoja na wageni kutoka sehemu mbalimbali waliokuja Makkah kufanya Umra.

Ikawa watu wanapishana, hawa wanatoka na wengine wanaingia. Pia Abdallah Bin Abbas na Talha Bin Zubair nao walifika kumuona Imam Husein (a.s).

Wawili hawa walimtaka Imam Husein (a.s.) akae hapo Makkah na anyamaze. (Asijihusishe na mambo ya Ukhalifa).

Swahili

Majlis Ya 5: Kumtolea Sadaka Maiti

Hapana shaka kwamba, ni jambo zuri kuwatolea sadaka maiti wa Waumini kwani jambo hilo alilifanya Mtume (s.a.w.) na akaamuru lifanywe.

Swahili

Majlisi Ya 4: Vikao Kwa Ajili Ya Kuhuzunikia Wafu

Hapana shaka kwamba Mtume (s.a.w.) alihuzunika huzuni nyingi kwa ajili ya kufiwa na Ami yake Bwana Abu Talib na Bibi Khadija Ummul-Mu'uminin (a.s.), kwani wawili hawa walifariki ndani ya mwaka mmoja, na Mtume akauita mwaka huo kuwa ni mwaka wa "huzuni."

Kipindi hiki cha msiba huu mkubwa, Bwana Mtume (s.a.w.) alipunguza kutoka, ikawa muda mrefu hukaa nyumbani, na ikawa Maquraishi wanapomhujumu huomboleza kwa kusema: "Ewe Ammi yangu imekuwa mapema mno kukukosa."

Taz. Siratul-Halabiya Uk.462 Juz.1.

Swahili

Majlisi Ya 3: Kusomwa Habari Za Waliokwisha Pita Hapo Kale

Hapana shaka kuwa, upo mkazo na umuhimu mkubwa kusoma na kueleza habari na sifa za waumini waliokwisha fariki zamani, na pia kutaja matatizo na misiba iliyowafika katika maisha yao ya kueneza Uislamu. Kwani kuyataja mambo yao huwa sawa kama kuwataja wao katika hali ya uhai wao.

Ummah hunufaika kutokana na utukufu walioupata zinapotajwa sifa zao, pia tabia njema walizokuwa nazo na vitendo vyao vizuri hunufaisha Ummah wa Kiislamu.

Swahili

Majlisi Ya 2: Ruhusa Ya Kuomboleza

Hapana shaka kwamba ipo ruhusa ya kuomboleza vifo vya Waumini, na kwamba jambo hilo ni halali, na hapana dalili iliyo kinyume cha hivi.

Kwa hakika baba yetu Nabii Adam (a.s.) aliomboleza kifo cha mwanawe Habil, na maombolezo yakawa yanaendelea mpaka leo kila inapotokea jambo la kifo katika kizazi cha wanaadamu bila upinzani.

Ama Mtume Muhammad (s.a.w.) aliwaruhusu Masahaba wake kufanya maombolezo kwa wingi kutokana na huzuni, na pia aliruhusu kutaja mema ya waliofariki na kutoa sifa zao katika tabia nzuri na matendo mazuri.

Swahili

Majlisi Ya 1: Ruhusa Ya Kulia

Hapana shaka kwamba kuwalilia wafu Waumini ni jambo linalofaa katika Uislamu kutokana na dalili ya kitendo cha Mtume (s.a.w.) kuhusu jambo hilo.

Swahili

Dibaji

Mtukufu Mtume (s.a.w.) asema:

"Ee Allah! Hawa (Ali, Fatima, Hasan na Husein) ndio Ahlul-Bayt wangu, basi watoharishe kwa tohara kamili."

"Husein anatokana na mimi na mimi ninatokana na Husein..."

"Hao (Hasan na Husein) ni maua yangu katika dunia."

"Ewe Mwanangu (Husein)! Mwili wako ni mwili wangu na damu yako ni damu yangu.."

Swahili