Sehemu ya 7
اللّهُمَّ رُدَّ كُلَّ غَرِيبٍ
Maana ya ‘Ghariib’
Kutokana na ujuzi mdogo wa baadhi ya tamaduni na lugha, baadhi yetu tunadhani kwamba neno ‘Ghariib’ lina maana ya ‘maskini’. Kwa mfano neno hili kwa ki-Urdu lina tumiwa kuonyesha umasikini wa mtu, lakini linapo tumiwa kwa maana makhsusi, kama vile ‘Gharibul watan’ lina kuwa na maana nyingine.