Sanda Ya Maiti Iliyo Wajibu

Ni faradhi kuvishwa maiti mwanamume au mwanamke mkubwa au mdogo vipande vitabu vya nguo:

(1) Kanzu (2) Shuka (3) Shuka

(1) Kanzu: Bila kuishona, itobolewe sehemu ya shingo tu halafu kitumbukizwe kichwa. Kuanzia begani hadi nusu ya miguu kupita goti.

(2) Shuka: Kama anavyovaa mwanamume kutoka kitovuni

hadi magotini, na ni bora si wajibu kuanzia kifuani hadi chini ya magoti.

Swahili

Namna Ya Kumkafini (Kumvisha Sanda Maiti)

Baada ya kukatwa mapande hayo, kwanza utatandika ile shuka kubwa ya Namba 3: Na ndio ya kwanza, baadaye utatandika Kanzu Kanzu kwa kuikunjua upande mmoja, (na hii ni ya pili), baadaye utaliweka shuka kwa upana kwa kukunjua. Ukisha tandika yote hayo vipande vitatu vya vitambaa vilivyo wajibu, basi sasa atalazwa maiti juu ya mapande yote ya sanda.

Kwanza utamfunga shuka na kuondoa kile kitambaa ulichotumia wakati wa kumwoshea kuficha utupu wake.

Utaurejesha ule upande wa kanzu ulioukunjua kwa kupitisha kichwa cha maiti kwenye shingo.

Swahili

Kumsalia Maiti

Sala Ya Maiti: Lazima iwe baada ya kuvishwa sanda na kutia HUNUUT (KUPAKA KAFURI kwenye VIUNGO VYA KUSUJUDIA). Kuanzia maiti mwenye umri wa miaka sita (6) huwa faradhi kusaliwa sala ya maiti.

Sala ya maiti haina Adhana wala Kukimu na pia hakuna rukuu wala sijda, lakini inakusimama tu, na ina Takbira tano tu (badala ya sala tano za faradhi za kila siku). Hakuna shuruti ya kuwa na wudhuu lakini ni sunna kuwa nao. Ni sunna pia wakati wakutoa kila Takbira, anyanyuwe mikono hadi masikioni mwake yule mwenye kuswali.

Namna Ya Kumsalia Maiti:

Swahili

Adabu Na Sunna Za Kwenda Na Jeneza

Swahili

Namna Ya Kuzika

(1) Ni faradhi kaburi lichimbwe kiasi cha kumfunika huyo maiti asiweze kufukuliwa na wanyama na isiweze kusikilizana harufu yake atakapoharibika.

(2) Ni sunna kuchimba kiasi cha urefu wa binaadamu au uchimbe hadi shingoni.

(3) Alazwe katika ubavu wa kulia iwe sehemu yake yote yote ya uso, kifua, tumbo na miguu (mwili wake mzima umeelekea Qibla).

Na ya Sunna ni haya:

Swahili

Jariy-Datain

Ni sunna iliohimizwa sana kwa SHIA WA AHLUL-BAIT (A. S.) kuwekewa maiti vijiti viwili vibichi vya mti wa mtende, kiasi cha urefu wa kila kijiti kiwe mkono mmoja, ambao huitwa "JARIY-DATAIN". Huandikwa juu ya maiti hayo jina lake na Ia baba yake maiti na Shahadatain, na majina ya Maimamu kumi na wawili (a.s.). Maiti huwa haadhibiwi vijiti vinapokuwa vibichi mpaka kukauka.

Swahili

Namna Ya Kulakiniwa Maiti

Ni Sunna kulakiniwa (kukumbushwa jawabu la kuwajibu hao Malaika). Nako ni kusema huku ameweka mkono wa kulia kwenye bega la kulia la maiti, na mkono wa kushoto kwenye bega la kushoto, na mdomo kwenye masikio ya maiti huku anamtikisa: "IS-MAA IFHAM YAA Fulaan (utaje jina la maiti) mara tatu. Na kama hajui jina lake aseme:

Swahili

Hadhari Muhimu

Akiwa maiti ni mwanamke, basi katika Talkini pale mwanzo atasema, "IS MA-IY IF-HA-MIY YAA" jina la mwanamke (maiti) huyo na baba yake na kama halijui atasema, "YAA AMATAL-LAAH;" tena ataendelea na hiyo Talkini kwa kusema, "HAL AN-TI ALAL AH-DIL LADHIY FAA-RIQ- TINAA".

Swahili

Namna Ya Kufukia Kaburi

(a) KiIa aliyoko hapo atabaruku naye kwa kusukuma mchanga kwenye kaburi kwa mgongo wa mkono wake wa kulia, na mwengine kwa majembe. Hala hala jamaa zake maiti wasitie mchanga, na makruhu na huleta ugumu wa moyo kama ilivyopokewa hadithi Tukufu ya Mtume (s.a.w).

(b) Likishajaa kaburi linyanyuliwe kidogo kiasi cha kipimo cha vidole vinne wazi na kutandazwa kufanya kama mraba.

(c) Liwekwe alama ya kujulisha kuwa kaburi hili ni la nani.

Swahili

Salaat Ul Wah-Shi

Ni sunna usiku wa kwanza wa kuzikwa maiti kusali sala rakaa mbili kwa ajili ya yule maiti na namna yake ni kama hivi:

Unanuia moyoni kwamba nasali rakaa 2 salaatul-wahshi, katika rakaa ya kwanza baada ya suratul Faatiha (AL-HAMDU) utasoma Aayatul Kursi, na rakaa ya pili baada ya "AL-HAMDU" utasoma sura ya IN-NAA ANZAL-NAA mara kumi, na ukisha toa salamu. Utasema "AL LAA-HUM-MA SAL-LI ALAA-MUHAM MADINI WA AA-LI MUHAM-MAD WAB-ATH THA-WAA BAHAA ILAA QABRI (FULAN jina la maiti) unaweza kusali wakati wowote usiku huo, lakini ni bora baada ya sala ya 'ISHA.

Swahili