Sifa za Kuzitambua Hadith

Ili kuweza kuzitambua ni Hadith za aina gani zilizo za uongo, Ma’ulamaa wetu wametupatia dalili ambazo zitakazotujulisha usahihi na ukweli wa Hadith hizo na masharti ni kwamba mtu yeyote asijitumbukize katka kuzieneza na kuzisherehesha Hadith hadi hapo atakapoweza kuthibitisha kuwa zinastahili hivyo. Hapa tunawaleteeni kwa mukhtasari.

Swahili

Zaka na Sadaka Huongeza Neema

Faida kuu mojawapo ya kutoa Zaka ni kuongezeka kwa neema na baraka ya mali yetu iwapo itatolewa kwa kuzingatia kanuni na ustaarabu wa kutoa hivyo, na ni kinyume na mawazo na mipango ya ki-Shaytani, kwani mabakhili hufikiria daima kuwa kwa kutoa mali yao kwa ajili ya misaada na Sadaka na Zaka, basi mali yao hupungua na hivyo wanaweza kuwa masikini na kwa hakika hayo ndiyo mawazo na upotofu wa Shaytani.

Swahili

Sadaka Na Misaada

Swahili

Madondoo juu ya Sadaka

Hapa nitapenda kuzungumzia machache kuhusu Sadaka
Sadaka inalipia madeni na kuongezea neema kwetu,

Sadaka inatuepusha na mauti katika hali mbaya

• Siku ya Qiyama kutakuwa na jua na joto kali mno, lakini Mu’min atakuwa katika kivuli, nacho ni Sadaka aliyokuwa akiitoa.

• Toeni Sadaka asubuhi na mapema, ili balaa na matatizo yasiwafikieni katika siku nzima.

• Muwatibu wagonjwa wenu kwa kutoa Sadaka

• Kutoa Sadaka ni afadhali kuliko kumnunua mtumwa na kumfanya huru

Swahili

1. Isisitizwe Kutoa Sadaka kwa wenye Shida, Masikini na wenye Madeni

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa :
“Sadaka inalipia madeni na inaongezea katika barakah.”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa:
“ Sadaka inamepusha mtu na ajali mbaya.”

3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa:
“Mtu yeyote yule aliye mja wa Allah swt akiwa Mu’min na akatoa Sadaka, basi Allah swt baada ya kifo chake huyo mtu huwaweka vyema na kuwasaidia wananyumba yake katika hali njema.”

Swahili

2. Msaada kwa Waislamu ni Afadhali kuliko Hijja ya Sunnah

Kusaidia familia ya waislamu wenye shida ni afadhali kuliko kwenda hijja zilizo sunnah na kuwafanya huru watumwa.

Swahili

3. Kuwatolea Wagonjwa Sadaka ni Sunnah

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Muwatibu wagonjwa wenu kwa Sadaka, na muzuie maafa kwa kuomba dua na kutoa sadaka muongezee riziki zenu zipanuke, na kwamba Sadaka inawaepusheni na mitego ya mashetani sabini.”

Swahili

4. Kutoa Sadaka Kwa Niaba ya Wengine

Mtoe sadaka kwa niaba ya watoto wenu na watoto wenu watoe sadaka kwa mikono yao hata kama itakuwa kidogo kiasi gani.

1. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. aliulizwa na Sahaba mmoja :
“Ewe mwana wa Mtume wa Allah! Mimi watoto wangu wawili wamefariki na amebakia mtoto wangu mdogo.”
Kwa hayo Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. kamwambia:
“Basi toa Sadaka kwa niaba ya mtoto wako huyo.”

Swahili

5. Mtoe Sadaka Kwa Mikono Yenu Wenyewe

Mtoe sadaka kwa mikono yenu wenyewe hususani wananyumba watoe sadaka kwa mikono yao na wanayempa wamwombe, awaombee dua njemaa.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa:
“Kwa kutoa Sadaka kwa mkono wako mwenyewe basi unajiepusha na ajali mbaya, unajiepusha na balaa na maafa sabini na mitego ya mashetani sabini na ambamo kila shetani yuko anakuambia ‘ewe fulani! Usitoe Sadaka kamwe.”

Swahili

6. Kutoa Sadaka Kila Mara na kwa Wingi ni Sunnah

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa alimusia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s.; Ewe Ali! Ninakufanyia usia wa mambo mema machache na uyakumbuke vyema".

“Ewe Allah swt umsaidie 'Ali” Baada ya hapo wakati akifanya usia, Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alisema: “Ama kuhusiana na sadaka, tafadhali usiwe na mnun’guniko wowote. Utoe kiasi kwamba mpaka uhisi kwamba wewe umefuja mali yako, lakini utambue wazi kuwa hiyo sio ufujaji bali hiyo umetoa katika njia ya Allah swt.”

Swahili