37. Namna Amali Njema ya ‘Kusaidia’ Inaweza Kuharibika
Si vyema kumsema mtu baada ya kumsaidia au kumsema yule uliyempa sadaka.
• Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa akisema:
“Allah swt amechukia na hafurahishwi na sifa sita na vile vile mimi sizifurahii hizo sifa sita na ndio nimefanya usia kwa mawasii na wafuasi waumini wote kuwa vitu hivyo sita wajiepushe navyo na mojawapo ni kule baada ya kutoa sadaka mtu akaanza kumsema yule aliyepokea (hiyo sadaka).