7. Katika Kutoa Sadaka Hata Kiasi Kidogo Chochote Kile ni Sunnah

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. anasema kuwa kuna riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa
“Toeni Sadaka, angalau hata kwa sa’ ya tende, na kama sa’ moja hiyo hamnayo basi mtoe tende kwa kiganja kimoja na hata kama hivyo haitawezekana basi mtoe tende kiasi chochote kile na kama hivyo haitawezekana basi mtoe angalau kokwa moja ya tende, na kama hivyo pia haitawezekana basi yule masikini aliyekuja kuwaomba, mumwambie maneno mazuri na matamu na maneno matakatifu katika kumwelezea kuwa hakuna chochote, na hayo pia ni sadaka.

Swahili

8. Kila Siku Asubuhi Mtoe Sadaka na Mnuie

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa:
“Toeni Sadaka asubuhi na mapema kwa sababu kunaondoa balaa kwa siku nzima.”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Kwa kutoa Sadaka asubuhi na mapema basi mtoa Sadaka huepukana na kila aina ya matatizo na mabaya yote kwa siku nzima.”

Swahili

9. Sadaka Huondoa Balaa ya Kila Aina

Kama kuna hofu ya kuja kwa balaa ama kwa kutokezea ubaya wowote au kwa sababu ya ugonjwa na hofu yoyote basi toeni sadaka.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ameripoti riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ambaye amesema:
“kwa baraka za Sadaka Allah swt humwondolea mwenye kutoa Sadaka balaa sabini, ambamo kuna magonjwa, madhara yatokanayo na moto, kuzama maji, kufunikwa na majumba mpaka kufa na atamwepusha ili asiwehuke au asiwe mwehu.”

Swahili

10. Sadaka Huepusha Hatari Katika Mali

Mnapokuwa na hofu ya kupata hatari katika mali, basi mtoe sadaka na kama hampati yule aliyemustahiki, basi mfanye nia sehemu hiyo muitenge na mali yenu.

Al Imam Hasan al-'Askary a.s. anasema kuwa:
“Wakati mmoja Al-Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akiwa pamoja na wenzake walikuwa safari na wenzake hao walikuwa na mali nyingi sana. Na njiani wakapata habari kuwa wako majambazi wanaowapora matajiri mali zao. Kwa kusikia hayo, hao matajiri walianza kutetemeka na wakaingiwa na hofu na wakaanza kumwuuliza Al-Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. Je! tufanyeje sasa?

Swahili

11. Waombaji Wanatakiwa Waridhike kwa Kile Wanachopata

Waombaji wanatakiwa waridhike kwa kile wanachopata, ni sunnah kuwaongezea wale walioridhika na kutowajali wale wasioridhika.

Siku moja Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alikuwa Mina pamoja na Ma-Sahaba wake, wakila zabibu. Mara akatokezea mtu mmoja na akaomba. Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kwa mkono wake akachukua fungu moja la zabibu akampa basi huyo akakataa kupokea, akisema “mimi sitaki zabibu hizi bali ninataka pesa tasilimu kama zipo ndio nichukue”.

Swahili

12. Ufahamu ya Muda au Masaa ya Kutoa Sadaka

Asubuhi na mapema na usiku unapoingia na saa zinazokuwa mbaya unapotoka nje basi mtoe sadaka.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“ Mimi nilinunua ardhi pamoja na mtu mmoja. Mtu huyo huyo alikuwa ni mnujumi, kwa hiyo yeye kila alipokuwa akipiga mahesabu yake na elimu ya nyota yake aliyokuwa nayo, alikuwa akiangalia saa nzuri ndipo alipokuwa akienda shambani mwake, nami bila kujali kama saa mbaya nilikuwa nikienda shambani mwangu, na sisi tulipokuwa tayari basi ardhi au sehemu yangu ikawa na faida zaidi kuliko sehemu yake.

Swahili

13. Ni Vyema Kutoa Sadaka Kifichoficho Kuliko Kidhahiri

1. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa akisema kuwa:
“Kwa kutoa Sadaka kifichoficho ghadhabu za Allah swt hupoa.”

2. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:
“Sadaka inayotolewa kidhahiri, basi kuliko hiyo Sadaka inayotolewa kifichoficho ni afadhali zaidi.”

Swahili

14. Kutoa Sadaka Usiku ni Sunnah

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. daima alikuwa akitoka usiku katika kiza huku amejitwisha mafurushi ya mapesa na vyakula kwa ajili ya kwenda kugawa kwa masikini katika mji wa Madina, na kuwafikishia misaada wahitaji. Na siku ambayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliaga dunia, watu wakaona hawakufikiwa na misaada hiyo ndipo walipojua kuwa misaada hiyo ilikuwa ikiletwa na Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ambaye daima alikuwa akificha uso wake ili watu wasijue kuwa ni yeye anayewafikishia misaada hiyo.

Swahili

15. Fadhila za Kutoa Sadaka Katika Siku Tukufu

Mujipatie fadhila kwa kutoa sadaka katika siku tukufu na mwezi wa Ramadhani.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Kutoa Sadaka siku ya Ijumaa kuna thawabu na fadhila kubwa sana.”

2. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. amesema:
“Msimkatalie masikini anayeomba siku ya ‘Arafah. Lazima mpeni chochote kile.”

3. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Mtu yeyote atakaye kuwa ametoa Sadaka katika mwezi mtukufu wa Ramadhani, basi yeye atakuwa ameepukana na balaa za aina sabini.”

Swahili

16. Je! Sadaka Itolewe Wakati Gani?

1. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alikuwa ameulizwa na mmoja wa Ma-Sahaba wake,
“Ewe Mtume wa Allah swt! Ni Sadaka ipi iliyo bora kabisa kuliko zote!”
Kwa hayo Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. alijibu:
“Sadaka iliyo bora ni ile ya wakati ule ambapo mtoa Sadaka yuko salama u salimini, mwenye afya kamili na anayeishi maisha mema bila wasiwasi, na ambaye anauogopa umasikini.

Swahili