27. Kumsaidia Mu’umin ni Sunnah

Kutoa katika mali yako kwa ajili ya kumsaidia mu’umin ni sunnah.

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa:

“Allah swt amefaradhisha kwa waja wake kwa kusisitiza kuwa kama yafuatavyo,
    • kwanza uadilifu na mapenzi yake pamoja na mu’min mwenzake kama vile ajipendeavyo yeye kwa ajili yake ndivyo ampendee mu’min mwenzake.

    • pili awe ameweka hisa fulani au kiasi fulani katika mali yake kwa ajili ya kutaka kumsaidia mu’min ndugu mwenzake. Na

Swahili

28. Baada ya Kutimiza Mahitaji ya Familia, Wasaidiwe Wengine

Mtu ambaye amesha timiza mahitaji ya watoto wake na ndugu na jamaa zake basi inambidi ajitaabishe nafsi yake kwa kuwahudumia wengine, hata kama huduma hiyo itakuwa ni bure lakini ni sunnah.

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. aliulizwa na mtu mmoja :

“Ewe Mawla! Je! ni mtu gani mwenzi wako aliyebora kabisa?”

Kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. alijibu,
“Ni wale ambao wanawawia na kuwafanyia mema ndugu zao katika imani katika hali ya raha, starehe na shida.”

Swahili

29. Sadaka Itolewayo Kwanza Inakwenda Katika Mikono ya Allah Swt

Ni sunnah kuubusu mkono wako mwenyewe baada ya kutoa sadaka na kukinusa kitu na kukibusu kitu ambacho unakitolea sadaka.

Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. Amenakiliwa hadithi yake moja

isemayo kuwa:
“Wakati muwapapo sadaka masikini muwaombe wawaombeeni dua, na akaendelea kusema, baadaye kuubusu mkono wa yule uliyemsaidia (uliyempa sadaka) kwa sababu sadaka unayoitoa kwanza inakwenda katika mikono ya Allah swt ndipo inapoingia katika mikono ya mwombaji.

Swahili

30. Ni Sunnah Kukopa

Katika kutoa sadaka ni sunnah kukopa na kumlipa maradufu aliyekukopa wakati wa kutoa sadaka.

1. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. siku moja aliijiwa na mtu mmoja ambaye akasema:

“Je! kuna yeyote yule atakayeweza kunisaidia kwa kunikopesha? Mmoja katika Ma-Ansaar akainuka na kusema :
‘Ewe Mtume wa Allah ! Mimi nina uwezo wa kumkopesha”.

Swahili

31. Ni Haramu Kuomba Kama Hakuna Haja

1. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:
“Mtu yeyote atakayeomba chochote bila ya kuwa na dharura yake, basi Allah swt atamfanya awe muhtaji kwa maswala hayo kabla ya kufa kwake, na kwa sababu ya kuomba kwake huku kusikostahiki, yeye ataadhibiwa na kutupwa Jahannam 1.”

Swahili

32. Maovu ya Kuomba Hata Kama Itakuwa ni Kijiti au Maji

1. Muhammad bin Muslim ameripoti riwaya kutoka kwa Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. kuwa amesema:
“Ewe Muhammad! Kama mwombaji (laiti) angelijua kuwa katika kuomba maovu mangapi yamejificha ndani yake, basi kamwe asingenyoosha mikono yake katika kuomba.”

Swahili

33. Kuomba Katikati ya Umati wa Watu si Vyema Kabisa

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema:
“Enyi watu! Msiombe wakati watu wanapokuwa katika makundi, isitokee kwamba kwa sababu ya ubahili wao ikawawia nyie machungu.”

Swahili

34. Uombaji

Mufadh-dhal bin Kais bin Rumman anasema kuwa:

“Yeye siku moja alikuwa katika huduma ya Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s., na mimi nikamdokezea kidogo kuhusu matatizo niliyokuwa nayo. Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. akamwambia kijakazi wake:
Naomba ule mfuko. Na akaniambia Abu Ja’afar (Manthur) amenitumia hizi Dinar mia nne kwa ajili ya msaada, hivyo chukua wewe. Na uende ukamalize shida na dhiki uliyo nayo.”

Swahili

35. Ruhusa Kumwambia Shida Zako Mu’umin

Kuruhusiwa kumwambia shida zako mu’umin na ndugu pale inapotokea.

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakiliwa katika riwaya moja amesema kuwa:

“Itakapo tokea miongoni mwenu mtu akazingirwa kabisa kwa hali mbaya, basi inambidi awajulishe jamaa na ndugu zake na asiiweke nafsi yake katika shida.”

Swahili

36. Heshima ya Mu’min ni Kule Kutokuwa Mwombaji wa Watu

Kuishi na watu kwa wema ni sunnah na kutokuwa na tabia ya kuwaomba omba wala kuwa na tamaa kwa yale waliyo nayo.

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amesema:

“Heshima ya muumin ni kule kuamka kwa ajili ya sala za usiku, na vile vile heshima yake ni kule kutokuwa mwombaji wa watu.”

Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. amenakili riwaya kutoka kwa Al Imam 'Ali bin Abi Talib a.s. kuwa amesema:

Swahili