47. Kulisha Chakula ni Sunnah

1. Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. ameripoti riwaya kutoka kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. kuwa amesema:
“Katika vitu vya kuleta uokovu mojawapo ni kuwalisha chakula wale wenye kuwa na shida na dhiki, na pili mtu awe ni mwanzilishi, awe ni mwanzo wa kutoa salamu na vile vile wakati watu wamelala usingizi mtu anaamka kwa ajili ya kusali na kufanya ‘ibada.”

Swahili

48. Mtoe Sadaka Kutoka Vile Vitu Mnavyovipenda Sana

1. Al-Kulayni anaandika riwaya kuwa Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. :
“Ilikuwa ni tabia yake kuwa alikuwa kila alipokuwa akikaa kula alikuwa ana beseni moja ambamo alikuwa akiweka kila aina chakula iliyokuwa mbele yake kidogo kidogo na alikuwa akitoa hukumu kuwa beseni hiyo ipelekwe kugawiwa kwa wenye shida na muhitaji. Na hapo akasoma ayah ya Qur'an Tukufu ifuatayo: Surah Al Balad, 90, ayah 11:
“Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.”

Swahili

49. Sadaka Mmoja Bora ni Kuutuliza Kiu cha Maji

Imesisitizwa mno kuwanywesha maji wanaadamu na wanyama hata kama hapo kutakuwa na maji mengi mno.

1. Al-Kulayni amemnakili Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. ambaye naye amemnakili Al Imam Muhammad al-Baqir a.s. riwaya kuwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. amesema:
“Siku ya Qiyama tendo jema kabisa malipo yake watapewa wale
watu ambao wamefanya wema katika kugawa maji.”
Riwaya hiyo hiyo Sheikh Saduq a.s. ameielezea pia.

Swahili

50. Kuwafanyia Hisani na Wema Ndugu Zetu Katika Imani

Ni sunnah kuwatendea mema waumini na kuwatimizia mahitaji yao kwa uwezo alionao mtu na kuwa na uhusiano mwema pamoja na mashi’a wenzake.

1. Al Imam 'Ali ar-Ridha a.s. amesema:
“Yeyote yule ambaye hakubahatika kutufanyia sisi wema basi ni wajibu wake kuwafanyia mema na kuwatimizia mahitaji ya marafiki zetu. Na yeyote yule ambaye hakubahatika kudhuru makaburi yetu basi adhuru makaburi ya wafuasi na marafiki zetu.”

Swahili

51. Inaruhusiwa Kutoa Sadaka Katika Hali ya Ruku’u, bali ni Sunnah

1. Sheikh Kulayni amenakili riwaya kutoka kwa Ahmad bin ‘Isa kuwa Allah swt amesema katika Qur’an Tukufu, Surah Al Maida, 5, Ayah 55:
‘Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, ambao hushika Sala na hutoa Zaka nao wananyenyekea.’

Swahili

52. Kugawa Nusu ya Mali Katika Sadaka ni Sunnah

Halabi anasema kuwa yeye alipomwuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq a.s. basi Imam a.s. akamjibu:
“Naam kabisa! Al Imam Hasan ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. aligawa nusu ya mali yake katika njia ya Allah swt – hadi kwamba nguo kwa nguo, Dinar kwa Dinar, alivigawa vyote katika njia ya Allah swt, na alikwenda Hija ishirini kwa kutembea na miguu.”

Swahili

Marejeo Ya Sadaka Katika Qur’an Tukufu

Na MAUDHUI SURAH : AYAH
1 ‘Ibada katika Sadaka 2:261; 2:262; 2:265; 2:272; 9:99; 76:9; 90:6
2 ‘Ibada na Sadaka 22:35
3 Asili ya Sadaka 4:78; 4:79
4 Athari za Sadaka
Swahili

Utangulizi Wa Mchapishaji

Kitabu hiki kilichoko mikononi mwako hivi sasa ni juhudi ya miaka mingi sana ya watu waliojitolea kuona kazi hii imefanikiwa bila ya kumsahau Marhum Abu Muhammad wa London.

Kama lilivyo jina la Tafsiri ndivyo ilivyo Tafsiri yenyewe ambayo mwanachuoni huyu mahiri kabisa aliyeifafanua ni mtu aliyebobea katika fani zote ambazo mfasiri (Mfafanuzi) anatakiwa awe nazo.

Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya ameonesha cheche zake katika vitabu vingi alivyoviandika katika maudhui mbalimbali na hivyo kujipa­tia wasomaji wengi sana.

Swahili

Sura Ya Sabini Na Nane: An-Nabai

Imeshuka Makka Ina Aya 40.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

عَمَّ يَتَسَاءَلُونَ {1}

Ni lipi waulizanalo.

عَنِ النَّبَإِ الْعَظِيمِ {2}

Swahili

Sura Ya Sabini Na Tisa: An-Naziaa’t

Imeshuka Makka Ina Aya 46.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure­hemu.

وَالنَّازِعَاتِ غَرْقًا {1}

Naapa kwa zinazotoa kwa nguvu.

وَالنَّاشِطَاتِ نَشْطًا {2}

Swahili