Dajjal

Ni neno la Kiarabu likimaanisha mhaini mkubwa na mleta balaa kubwa mno.Hivyo wale wote walio wahaini na waleta balaa basi wajijue kuwa wao pia na ma-Dajjal wa zama zetu hizi.Lakini Dajjal anayezungumziwa hapa ni yule ambaye anaitwa Sayyid na utambulisho wake ni Dajjal.Yeye atakuwa ni mchawi mkubwa.Hapo mwanzoni atakapojitokeza atadai kuwa yeye ni mtume na baadaye atajiita kuwa yeye ni mungu.Yeye atatokezea pale ambapo Mashariki ya kati itakuwa imekwisha dhoofika kwa sababu ya ukame utakaodumu kwa miaka mitatu kwa mfululizo.

Swahili

Dibaji

Namshukuru Mwenyezi Mungu. Ule waadi niliotoa katika gazeti letu la "Sauti Ya Bilal", la mwezi Sept. 1974, toleo Ia No. 5, nilisema, nitaandika kitabu kizima kuhusu mambo anayofanyiwa Maiti kwa kirefu Inshallah, Alhamdulillah Mwenyezi Mungu kwa baraka ya Muhammad na Aali zake watakatifu [s] kautimiza kwa kunipa tawfiki ya kuchapisha kitabu hiki.

Swahili

Kuhusu Mambo Ya Maiti

Mwenyezi Mungu katika Qur'ani Tukufu, sura ya 'TABARAKA' Aya ya kwanza na ya pili, Amesema hivi "Ametukuka yule Ambaye Mkononi mwake umo ufalme wote; naye ni Mwenye uwezo juu ya kila kitu. Ambaye Aliumba kifo na uzima ili kukujaribuni (kukufanyieni mtihani); ni nani miongoni mwenu mwenye vitendo vizuri zaidi. Naye ni Mwenye nguvu na Mwenye Msamaha. (67:1 na 2).

Swahili

Hukumu Katika Hall Ya "Ihtidhaar" (Kukata Roho)

Mambo anayofanyiwa mtu anapokata roho na baadaye: Mwislamu anapofika katika hali ya Ihtidhari (wakati wa ukata roho), mwanamume au mwanamke, mkubwa au mdogo; ni wajibu (ni fardhi) kwake kama anajiweza na anayo fahamu na kama si hivyo basi kwa wale watu waliohudhuria hapo wamlaze huyo mgonjwa chali, miguu na nyayo zake zielekee Qibla, na ikiwa haimkiniki kufanya hivyo kwa ukamilifu basi kadri itakavyomkinika waanye, na ikiwa haimkiniki kabisa basi wamkalishe kuelekea Qibla. Na kama hiyyo pia haimkiniki basi wamlaze mkono wa kulia au wa kushoto kuelekea Qibla.

Swahili

Hukumu Baada Ya Kufa

Baada ya kufa ni sunna, (1) Kufumbwa macho yakiwa wazi (2) Kuzibwa kinywa kwa utepe utakaopitishwa chini ya taya na kufungwa tanzi juu ya kichwa, (3) Kunyooshwa mikono, miguu na mapaja yake, (4) Kufunikwa shuka na kama amekufa usiku, mahala hapo pawashwe taa wasimwache maiti kizani, (5) wapashwe wenye imani (Waislamu) majira za mazishi ili waweze kuhudhuria mazishi yake, na wafanye haraka upesi kuzikwa.

Swahili

Hukumu Za Kumwosha Maiti

Ni fardhi juu ya kila Mwislamu kumwosha maiti huyo, na kutengeneza mazishi yake yote, lakini wakishajitokeza watu kumshughulikia huyo maiti basi kwa wengine fardhi hiyo huondoka.

Ni haramu mwanamke kuoshwa na mwanamume, au mwanamume kuoshwa na mwanamke, lakini mke ana weza kumwosha mume hata kama wapo wanaume, na mume anaweza kumwosha mke hata ikiwa wapo wanawake wa kumwosha.

Mwanamume anaweza kumwosha mtoto wa kike asiyezidi miaka mitatu, na pia mwanamke anaruhusiwa kumwosha mtoto wa kiume asiyezidi miaka mitatu.

Swahili

Sunna Za Kumwosha Maiti

Awekwe mahala palipo juu, kama kitanda, au baraza n.k. na mahala pa kuwekea kichwa chake painuke zaidi kuliko miguu.

Alazwe chali, miguu na nyayo zielekee Qibla (kama tulivyotaja katika mambo ya hali ya 'IHTIDHARI'.

Maiti avuliwe nguo zote kwa upande wa chini (miguuni) hata ikibidi itatuliwe (ichanwe) lakini kwa idhini ya warithi wa maiti.

Aoshwe chini ya sakafu, au banda au hema asioshwe chini ya mbingu.

Uchimbwe "UFUO" wa kuingia maji ya kuoshea.

Mwili wake wote uwe wazi isipokuwa utupu wake.

Swahili

Utaratibu Wa Kumwosha Malti

(a) Baada ya kusafishwa mwili wake wote kwa sabuni (au kitu kingine) na kuondoshwa uchafu wa aina yo yote kama (madawa, marhamu au mafuta) ndipo huyo mwoshaji Mwislamu atamwosha ghusli tatu (mara tatu kuoshwa). Ni sunna kabla ya kuanza kumwogesha maiti ghusli tatu, atamwosha mikono yake mara tatu, kwa kila ghusli.

Swahili

Namna Ya Kumwosha Maiti

Baada ya kusafishwa mwili wote wa yule maiti hapo (yule mwoshaji) atanuia kuwa, namwosha (huyu maiti) ghusli ya kwanza kwa maji yaliyochanganyishwa na majani ya mkunazi kama tulivyoeleza huko nyuma.

(a) Kwanza ataanzia kwa kummwagia maji kichwani (maji yafike hadi utosini kwenye ngozi) masikio, pua, mdomo, macho na shingo pia aoshe. Ahakikishe kilmara anapomwosha, maji yafike sehemu zote za mwili wake.

Swahili

Mambo Ya Faradhi Baada Ya Kuogeshwa Maiti Hadi Kuzikwa Kwake

Haifai wakati anapooshwa maiti kuweko moto au kiteso cha kufukiza wala wakati wa mazishi hadi mwisho.

Swahili