Mwenyezi Mungu (s.w.t.) katika Aya hii ametaja aina ya wanawake walio halali kwa Mtume (s.a.w.) na kumwachia hiyari ya kumlalia na kutomlalia anayemtaka. Kisha akamharamishia kuzidisha wale aliokuwa nao au kubadilisha mwingine. Wakati huo alikuwa na wake tisa. Ufuatao ni ufafanuzi:
Ewe Nabii! Hakika sisi tumekuhalalishia wake zako ambao umewapa ujira wao.
Enyi ambao mmeamini! Msiingie majumba ya Mtume ila mkipewa ruhusa ya kwenda kula, sio kungojea kiive. Lakini mtakapoitwa, basi ingieni. Na mkisha kula, tawanyikeni wala msiweke mazungumzo.
Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.
Kuna kauli nyingi kuhusu neno Jalbab: kuna wanaosema kuwa ni nguo inayomfunika mwanamke kutoka kichwani hadi nyayoni. Wengine wakasema ni ushungi unaofunika kichwa cha mwanamke na uso wake. Kauli hii ndio aliyo nayo mwenye Majmaul-Bayan.
Zimekwishatangulia Aya mbili zinazofahamisha wajibu wa hijabu kwa wanawake:
Enyi ambao mmeamini! Mcheni Mwenyezi Mungu na semeni kauli ya sawa. Atawatengenezea matendo yenu na atawaghufiria dhambi zenu.
Imeshuka Makka. Ina Aya 54.
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
الْحَمْدُ لِلَّهِ الَّذِي لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَلَهُ الْحَمْدُ فِي الْآخِرَةِ ۚ وَهُوَ الْحَكِيمُ الْخَبِيرُ {1}