Sura Ya Thelathini Na Nane: Saad
Imeshuka Makka Ina aya 88
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
Imeshuka Makka Ina aya 88
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
Swaad.
Umetangulia mfano wake katika Juz. 1 (2:1).
Naapa kwa Qur’an yenye ukumbusho, Lakini waliokufuru wamo katika majivuno na upinzani.
Baadhi ya wafasiri, wakifafanua Aya hii, wamemnasibishia Nabii Daud mambo ambayo si laiki hata ya mtu wa kawaida mwenye murua na haya; sikwambii tena mtume aliye maasumu. Wakataja kisa kirefu kutoka katika Biblia kitabu cha 2 Samweli: 11 na 12, kutoka agano la kale ambalo mahala pake pamechukuliwa na hukumu ya Qur’an. Nukuu za agano lenyewe kuhusiana na hilo haziingiliki akili.
Ewe Daudi! Hakika Sisi tumekufanya uwe Khalifa ardhini.
Kila mtu aliyeko, au atakayekuweko, ardhini basi huyo ni khalifa wa Mwenyezi Mungu ardhini; kwa maana yakuwa ana majukumu mbele ya Mwenyezi Mungu ya kufanya mambo ya heri duniani na Akhera katika maisha haya.
Na Daudi tukamtunukia Suleiman, mbora wa waja. Kwa hakika alikuwa mwingi wa kutubu.
Na mkumbuke mja wetu Ayyub
Huu ni ukumbusho.
Yaani huko kutaja Mwenyezi Mungu (s.w.t.), katika Aya zilizotangulia, sifa za manabii, kama Ibrahi, Ismail, Daud, Suleiman na wengineo.
Na hakika wenye takua wana marudio mazuri.
Sema: Hakika mimi ni mwonyaji tu; na hapana Mola ila Mwenyezi Mungu Mmoja, Mtenza nguvu. Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo kati yake, Mwenye nguvu, Mwingi wa maghufira.
Imeshuka Makka ina Aya 75 isipokuwa Aya tatu.
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ