36. Tawba Ndiyo Sababu Ya Kusamehewa
Allah swt anatuambia 'Saabiquu' yaani haraka haraka mtangulie. Je ni wapi huko tena? Basi jibu ni kuelekea kwake Allah swt, hiyo TAWBA inaweza kuwa sababu ya rehema za Allah swt. Faradhi na Sunna zote ni sababu za rehema na Maghfirah za Allah swt. Matendo yote mema ni wasila wa Maghfirah zake Allah swt. Iwapo utauondoa mwiba njiani basi iwe ni kwa ajili ya Allah swt, na ulifanyalo jambo lolote lile, liwe kwa ajili ya Allah swt na yawe yote kwa ajili ya kutaka radhi na maghfirah zake Allah swt.