26. Wenye Kutubu Hawatatoa Ushahidi Dhidi Ya Madhambi Yao

Ni jambo la kusikitisha mno kuwa sisi na nyinyi tutasimamishwa kwa pamoja mbele ya Allah swt kwa ajili ya kutolewa uamuzi baina yetu kuhusu matendo yetu. Imam Jaafer as-Sadique a.s. katika Usuli Kafi, mlango wa TAWBA anatubashiria kuwa:

Swahili

25. Moyo Wa Sheitani Hubabaika Kwa Istighfaar Za Watu

Iwapo mtu yeyote anataka kupigana na adui shetani, basi itambidi awe na silaha gani? Mtume Mtukufu s.a.w.w. anatuelezea amali mojawapo ambayo inaweza kumvunjia sheitani juhudi zake zote. Nayo ni ISTIGHFAAR (kutubu) ambayo inamfukuzia mbali shetani. Je ni nani miononi mwetu ambaye hajawahi kumtii na kumfuata sheitani? Wingi wa wakati wetu wa magomvi huwa tunamtii sheitani, je hasira na ghadhabu zetu zisizo na msingi au kutokuwa na huruma, si vyote hivyo ni vishawishi vya shetani?

Swahili

24.Toba Inaweza Kukubaliwa Kwa Kumtawasuli Imam Hussein

Sisi huwa daima tunaomba, "Ewe Mola wetu! Tujaalie Tawfiqi ya Toba ili tuweze kusamehewa madhambi yetu na kiza cha moyo wetu kuondoka."

Swahili

23. Kisa Cha Kijana Mwenye Madhambi

Ma'adh anasema: "Siku moja nilikuwa nkijiandaa kwenda kwa Mtume s.a.w.w. , na mara nikamwona kijana mmoja akilia mno, basi hapo nilimwuliza sababu ya kilio chake hicho. Huyo kijana alinibu kuwa yeye ni mwenye dhambi kubwa mno. Basi hapo nilimwambia aje pamoja nami kwa Mtume s.a.w.w. ili amwombee msamaha kwa Allah swt. Hapo huyo kijana alisema kuwa alikuwa akiona aibu kuja mbele ya Mtume s.a.w.w. kwa sababu ya dhambi zake." Hapo Ma'adh aliendelea na safari yake hadi kwa Mtume s.a.w.w. na kumwelezea yale yaliyotokea. Basi Mtume s.a.w.w.alimwambia akamlete yule kijana.

Swahili

22. Tawba Ni Nuru Ya Matumaini

"Ewe uliyekwisha tenda madhambi! Usikate tamaa kwa rehema za Allahs swt, rejeeni katika njia yake, na hataki muendelee kutenda madhambi vile mupendavyo na mutakavyo - tukidhani kuwa atatusamehe tu! La sivyo hivyo! Makusudi ya kutokata tamaa ni kwa wale waliokwisha tenda madhambi wakidhani kuwa hawana la kufanya kusamehewa hivyo wakaendelea na maasi yao, bali inawabidi waitambuw na waombe TAWBA na msamaha wa Allah swt. Hivyo wajue kuwa pale wanapotenda dhambi, waombe Toba mara moja. Inawezekana Allah swt akazikubalia TAWBA zetu.

Swahili

21. Tawba Ni Faradhi Baada Ya Kila Dhambi

Katika faradhi mojawapo za Muislamu ni kutubia mara moja pala anapotenda madhambi na hivyo ndivyo ilivyo wajibu. Iwapo atamwona mtu mwingine akitenda madhambi, basi amshawishi kutubu.

Swahili

20. Tusiwaite Watu Kwa Majina Mabaya Au Majina Ya Utani

Tusiwe na tabia ya kuwaita watu kwa majina mabaya na yale yaliyokuwa ya utani au mzaha. Mfano, iwapo mtu mmoja alikuwa 'Myahudi' hapo awali na baadaye akawa Mwislamu, basi haifai kamwe kumwita 'ewe mwana wa Kiyahudi.' Vile vile usimwite mtu 'mlevi' wakati amekwisha kufanya toba.

Ni lazima kabisa kuwaita Waislamu kwa majina yaliyo bora kabisa. Ni haramu kumwita Muumin kwa jina au sifa mbaya. Mfano "Ewe mfupi kama nyundo! au ewe ''Mfasiqi' ni jina baya kabisa (kwa yeyote) baada ya yeye kuwa Muislamu.'''

Swahili

19. Tuombe Tawba Kwa Madhambi Tuliyokwisha Tenda

Haitupasi kamwe kumdharau mtu yeyote wala tusimfanyie masihara wala tusimdhalilishe kwani hatujui iwapo huyo mtu yu mwema nyuma ya pazia za macho zetu. Bali inatubidi tuseme, labda yeye anazo tabia njema kuliko tabia zangu ambazo mimi sinazo, inawezekana yeye anazo heshima zaidi mbele ya Allah swt. Vile vile inawezekana kuwa mambo yake usiyoyapendelea wewe yakawa ni mema:
Huenda wakawa bora kuliko wao.

Swahili

18.Tuyateketeze Madhambi Yetu Kwa Tawba

Allah swt anatuambia katika Sura Hujuraat, aya 11:-

Na wasiotubu, basi hao ndio madhalimu. (49:11)

Sehemu hii ya mwisho wa aya hii inatubashiria na kutuitia katika TAWBA hivyo tuitikie mwito huo na tufanye TAWBA.

Allamah Iqbal anasema:"Matendo ndiyo yafanyayo maisha ya mtu yawe ya Peponi au Motoni, huyu kiumbe si wa peponi wala motoni alipoumbwa."

Swahili

17. Allah Swt Huzikubali Tawba

TAWBA ni mojawapo iliyo dharuri, na ambayo utekelezaji wake ni faradhi kwa kila Mwislamu. Allah swt amesema katika Sura an-Nuur, Aya 31:-

Na tubieni nyote kwa Mwenyezi Mungu, enyi Waislamu ili mpate kufaulu. (24:31)

Vile vile twaambiwa katika sura an-Aam, Aya 34:-

Swahili