46. Dua Ya Imam Zaynul Aabediin Katika Kuomba Tawba

Ewe Mola wangu, ambaye sifa za kukusifu za wenye kukusifu haziwezi kutajika. Ewe mwenye mategemeo ambaye mategemeo hayawezi kwenda zaidi yako.Ewe ambaye kwako wewe malipo ya waja wako hayatapotea. Ewe unayeogopwa na waja wako. Ewe uliye khofu ya mja wako na hii ndiyo nafasi imemkuba ghafla kwa madhambi.

Ambaye amevutwa na zama za makosa na ambayo yameghalibiwa na sheitani.

Kwa hivyo ameshindwa kabisa kutimiza yale uliyokuwa umemwamrisha kuyafanya na yeye hakuyafanya.

Swahili

45. Sifa Za Wamchao Allah

Ifuatayo ni Hotuba Na. 193 ya Imam Ali ibn Abu Talib a.s. kutoka Nahjul Balagha. (Sharh ya al- Hadid, Vol. 10, uk. 132-162)

Swahili

44. Aya Ya Qurani Zizungumziazo Tawba

Sura na Aya zifuatazo zinazungumzia TAWBA Qurani: (Kwanza inatangulia nambari ya sura na kufuatiwa kwa nambari ya Aya).

Swahili

43. Mazungumzo Ya Bahati

Imam Jaafer as-Sadique a.s. amenakiliwa katika Usuli Kafi akisema:
Mcha Mungu mmoja na fisiqi (mwenye madhambi) mmoja waliingia Msikitini kwa kufanya ibada. Walipotoka nje mambo yakawa yamebadilika kabisa yakawa kinyume.Yaani yule fassiq alipoingia Msikitini alivutiwa na ibada za huyo Mcha Mungu na hivyo aliathirika mno moyoni mwake. Hapo allah swt alipendezewa mno na hali yake hiyo. Lakini yule Mcha Mungu aliyekuwa anayo ghururi (majivuno) alipomwona yule Faasiqi huyu amejiingiza humu Msikitini miongoni mwetu sisi wenyewe kufanya ibada bora?"

Swahili

42. Msamaha Ndiyo Malipo Ya Istighfaar

Mfasiri mmoja wa Quran anasema:
a. Malipo ya TAWBA ni kukubaliwa kwake,
b. Malipo ya Istighfaar ni msamaha,
c. Malipo ya kushukuru ni kuzidishiwa neema,
d. Malipo ya Duaa ni kusikilizwa kwake,
e. Malipo ya sala ni kutimiziwa kwake,
f. Kwa kifupi Qurani inatuambia: Hakuna malipo ya wema ila wema tu! (55:60)

Swahili

41. Tawba Hutuepusha Na Moto Wa Jahannam

Imam Jaafer as-Sadique a.s. amenakiliwa riwaya moja katika Usuli Kaafi:
Siku moja Imam Ali ibn Abi Talib a.s. alimtembelea Sahaba mmoja na hapo alitokezea mtu mmoja akisema: "Ya Ali! Mimi nimetenda tendo la aibu pamoja na kijana mmoja (ulawiti), hivyo naomba nitakasike kwa mujibu wa Shariah za Allah swt."

Imam Ali a.s. alimwambia:"Kwa hivi sasa naomba uende zako kwani inawezekana ulitenda tendo hilo kwa ushawishi uliokuwa umekughalibuNa hivyo inawezekana kuwa akili zako hazikuwa timamu na maneno yako yasiwe yenye fahamu au maana yoyote."

Swahili

40. Tawba Ya Mauaji

Iwapo mwuaji anataka kufanya TAWBA, basi inambidi kwanza ajisalimishe mbele ya warithi wa marehemu aliyeuawa na hapo ni shauri lao wao iwapo watatekeleza kisasi au watadai fidia au watamsamehe.

Iwapo mtu ataua kwa makosa au kwa kumdhania mtu kimakosa basi ni lazima kwake yeye kulipa fidia kwa familia na warithi wake marehemu. Na iwapo wao watamsamehe, basi ni faradhi juu ya muuaji kumfanya huru mtumwa mmoja, kuwalisha masikini sitini na kufunga saumu kwa siku sitini kwa mfululizo. Kama haweza kumfanya huru mtumwa mmoja, basi avitekeleze vilivyobakia.

Swahili

39. Madhambi Yote Yanaweza Kusamehewa

Katika Qurani Tukufu zipo aya nyingi mno na vile vile zipo hadithi ambazo zinazungumzia ukubaliaji wa TAWBA na vile vile zielezeazo kuwa madhambi yote yanaweza kusamehewa. Katika Qurani Allah swt anajisifu kuwa yeye ndiye Msamehevu na mwenye kuzikubalia TAWBA na vile vile anajiita katika Qurani kwamajina tofauti tofauti: Tawwab, Ghaffar, Ghafirudh-Dhunuub..........

Swahili

38. Madhambi Ni Giza Wakati Tawba Ni Nuru

Allah swt anatuambia katika Qurani:

Mwenyezi Mungu ni mlinzi wa wale walio amini, yeye huwatoa kutoka giza na kuwaingiza katika nuru.....(2:257)

Imam a.s. anasema: "Kuongozwa kunamfanya mtu atolewe kutoka gizani na kuelekezwa penye maghfrah na ambavyo hatimaye TAWBA kamilifu."

Swahili

37. Mazungumzo Ya Imam Zaynul Aabediin Na Zahra

Imam Zaynul Aabediin a.s. alikuwa akielekea Makkah na aliliweka hema lake chini ya mlima mmoja ujulikanao kama 'Zahra.' Zahra alikuwa ni hakimu na pia alikuwa mfuasi wa Imam Zaynul Aabediin a.s. na alikuwa akimtembelea mara kwa mara.

Huyo Zahra siku moja alimhukumu mtu mmoja kifungo kwa makosa aliyokuwa ameyatenda, na kwa bahati mbaya huyo mfungwa alifariki akiwa kifungoni. Kutokana na tukio hilo, Zahra alijitoa hapo mjini Madina na kuishi katika mlima huo huu akilia na kujuta mno akiwa amewaacha mke na watoto wake wote.

Swahili