Hadithi Ya Jabir
Hadithi ya Jabir inafahamika kuwa ni miongoni mwa hadithi wanazozitegemea Mawahabi kuharamisha kujenga juu ya makaburi; na imepokewa hadithi hii katika Sihah na Sunan kwa matamko tofauti tofauti, na wanapatikana katika Sanadi zake zote na mapokezi yake wanapatikana watu wawili.
1. Ibnu Juraih
2. Abuz-Zubair.
Na ili kuthibitisha kusihi kwa hadithi hii itategemea kuzifahamu hali za wapokezi wake na watu wa Sanad yake.
Katika maelezo yafuatayo tutaitaja hadithi hiyo kwa matamko mbali mbali tena tofauti: