(3) Wanavyosema Wapinga Maulidi Na Majibu Yetu

Bado tunaendelea na hujja za wanaopinga maulidi.

Hujja yao ya tatu ni kuwa: kuweka ada ya kusoma maulidi ni kuigiza Wakristo walioweka siku ya Krismasi; na Mwislamu haruhusiwi kufanya hivyo.

Swahili

(2) Wanavyosema Wapinga Maulidi Na Majibu Yetu

Katika makala yetu kabla ya haya, tulijibu hujja ya kwanza ya wanaopinga maulidi. Leo tunaendelea na hujja yao ya pili.

Katika hujja yao ya pili wanasema: Maulidi hayakusomwa na maswahaba wala waandamizi wao (taabi'in). kama kweli yangelikuwa ni sawa kuyasoma, bila shaka mabwana wakubwa hao wangelikuwa ni wa mbele kufanya hivyo.

Swahili

(1) Wanavyosema Wapinga Maulidi Na Majibu Yetu

Katika makala yetu ya kwanza tuliahidi kuzijadili ki-ilimu, moja baada ya moja, hujja zinazotolewa na wanaopinga maulidi. Kwa hivyo leo tunaanza:

Hujja yao ya kwanza ni kwamba: maulidi hayakuwako zama za Mtume Muhammad (s.a.w.w.) Kwa hivyo, kuyaleta baada ya yeye kufariki dunia, ni bid'a (uzushi). Na kila bid'a, kwa maneno yake mwenyewe Bwana Mtume (s.a.w.w.), ni upotevu. Kwa hivyo, kila anayesoma maulidi amepotea!

Swahili

Sherehe Za Maulidi

Maulidi ni Kiswahili cha neno la Kiarabu, mawlid. Neno hili lina maana ya "mazazi" au "kuzaliwa kwa…" (birthday). Kwa kawaida, linapotumiwa na Waislamu, huwa na maana ya siku aliyozaliwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.), au hafla ya kuisherehekea siku hiyo.

Swahili

Khitamuhu Misk

Ewe msomaji mpendwa, sasa hivi umefika wakati wakuhitimisha uchambuzi huu mpana kuhusu itikadi za Kiwahabi na misingi yake na malengo yake kwa neno fupi lenye manufaa kwa jamii ya Kiislamu kwa jumla, na kwa vijana wa Kiislamu wenye ghera kwa upande wao.

Bila shaka Uislamu umejengwa juu ya maneno mawili:

Kalimatul-Tauhid na Tauhid-ul-Kalimah, basi ni wajibu juu ya umma wa Kiislamu kuulinda umoja wa kalima na mshikamano wa udugu, kama ambavyo ni wajibu juu ya umma kuihifadhi Kalimatul-Tauhid kwani viwili hivyo ni matawi mawili yanayotokana na asili moja.

Swahili

Uchambuzi Wa Mwisho

Hapa zimebakia sehemu mbili muhimu za uchunguzi tutazionyesha katika sehemu hii ya mwisho, nazo ni kama ifuatavyo:

A). Kumlilia maiti kabla ya kuzika au baada ya kuzika.

B). Kudhifia tamko la "Abdi" kwa mja.

Basi huenda mtu asiyejua hukmu za sheria akadhani kuwa, sheria zimeyaharamisha mambo hayo, na sasa hivi tunabainisha hukmu zake kwa mujibu wa kitabu (Qur'an) na sunnah na tunasema:

Kwanza: Kumlilia maiti:

Swahili

Malengo Ya Hijja Ya Kisiasa Na Kijamii Katika Kauli Za Wanachuoni

Kwa hakika wanachuoni na wanafikra wengi wa Kiislamu wameandika umuhimu wa Hijja kisiasa na kijamii na wakazingatia kuwa ni msimu bora na fursa nzuri kwa Waislamu kuonyesha nguvu yao, mshikamano wao, muamko wao na umoja wao kwa kauli na matendo na kwa dhahiri na hisia.

Basi huyu hapa Al-Allamah Muhammad Farid Waj-di anaiandika ndani ya Dairatul-Maarif yake Maddah ya Hijja anasema:

Swahili

Hijja - Msimu Wa Ibada Na Ni Mkutano Wa Kisiasa

Mwenyezi Mungu ameifanya al-Kaaba kuwa ni nyumba tukufu na ni wasila wa kusimamisha amani miongoni mwa watu, na akaifanya Hijja kuwa ni msimu wa ibada na ni fursa ya Waislamu kutoka kila upande kukutana na kufahamiana, na pia wafahamishane mambo muhimu ya Dini yao na kuzichunguza hali zao.

Basi mambo haya baada ya Ibada ni miongoni mwa uthibitisho dhahiri wa kauli ya Mwenyezi Mungu aliposema:

"Na ili washuhudie manufaa yao…" Qur'an, 22:28.

Swahili

Kuwaomba Msaada Mawalii Wa Mwenyezi Mungu

Je, inafaa kuwaita Mawalii wa Mwenyezi Mungu kuwaomba msaada wakati wa shida na matatizo?

Mas-ala haya ni miongoni mwa Mas-ala ambayo kuna tofauti ndani yake baina ya Waislamu na Mawahabi.

Kuwaomba msaada Manabii na Mawalii wa Mwenyezi Mungu, na pia kuwaita kwa majina yao wakati wa shida, matatizo na mambo ya hatari ni sunna iliyojengeka miongoni mwa Waislamu.

Swahili

Kumuapia Asiyekuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu

Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni miongoni mwa mambo ambayo Mawahabi wana uchungu nayo sana na ni katika mas-ala ambayo wao wanayakemea na kuyapigia kelele kwa kutumia kalamu zao potofu.

Mwandishi wa Kiwahabi aitwaye As-San-Ani, yeye kwa mawazo yake anaona kuwa kumuapia asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni shirki!!1

Swahili