Orodha Ya Vitabu Vilivyo Chapishwa Na Al-Itrah Foundation

1. Qur'an Al-Kariim - Tafsir Al-Kashif Juzuu ya kwanza mpaka Ishirini na Nne
2. Uharamisho wa Riba
3. Uharamisho wa uwongo Juzuu ya kwanza
4. Uharamisho wa uwongo Juzuu ya pili
5. Hekaya za Bahlul
6. Muhanga wa Imamu Husein (A.S.)
7. Mikingamo iliyomzunguka Imamu Ali (A.S.)
8. Hijab vazi Bora
9. Ukweli wa Shia Ithnaashari
10. Madhambi Makuu
11. Mbingu imenikirimu
12. Abdallah Ibn Saba

Swahili

Somo La Kumi Na Tisa: Urithi Wa Az-Zahrau (A.S.)

i. Imepokewa toka kwa Fatima binti wa Mtume (s.a.w.w.) kuwa yeye Fatima aliingia nyumbani kwa Mtume (s.a.w.w.), hapo Mtume (s.a.w.w.) akatandika nguo kisha akamwambia akae juu yake, kisha akaingia Hasan, Mtume (s.a.w.w.) akamwambia kaa pamoja na mama yako. Akaingia Husein, Mtume (s.a.w.w.) akamwambia kaa nao. Kisha akaingia Ali (a.s.) akaambiwa na Mtume (s.a.w.w.) kaa nao.

Swahili

Somo La Kumi Na Nane: Fadhila Na Mwonekano Wa Az-Zahrau (A.S.)

Imani Na Ibada Zake Kwa Ajili Ya Mwenyezi Mungu

Kumwamini Mwenyezi Mungu ndio alama ya mwanadamu mkamilifu, na ibada kwa ajili ya Mwenyezi Mungu ndio ngazi ya kufikia kilele cha ukamilifu. Na hakika manabii wamepata makazi bora katika nyumba ya heshima kutokana na daraja lao la imani na juhudi zao za kuchuma mema hapa duniani na moyo mkunjufu katika ibada kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.

Swahili

Somo La Kumi Na Saba: Fadhila Na Mwonekano Wa Az-Zahrau (A.S.)

Hakika yeye ni binti wa nabii aliyezikomboa na kuziongoza akili zama zote. Pia yeye ni mke wa Imam ambaye alikuwa nguzo miongoni mwa nguzo za haki na mwendelezo wa nabii mtukufu katika historia ya mwanadamu.

Hakika Fatima (a.s.) alipata akili kamilifu, roho nzuri, na dhamira safi, hivyo kwa msimamo wake na urithi wake akatuchorea sifa za njia bora ambayo dini imepita. Hivyo yeye Fatima (a.s.) akawa nguzo kati ya nguzo za dini, kwa ajili hiyo huwezi kujua historia ya Uislamu vizuri bila kujua historia yake.

Swahili

Somo La Kumi Na Sita: Mwonekano Wa Utu Wa Fatima Az-Zahrau

Fatima Az-Zahrau (a.s.) ni binti wa nabii mtukufu na ni mke wa Imam mtukufu na ni mama wa wajukuu wawili Hasan na Husein mabwana wa vijana wa Peponi. Hakika yeye ni uso wenye kung’ara kwa ajili ya utume wa mwisho, na ni chombo safi kwa ajili ya kuendeleza kizazi kitakasifu, na ni chimbuko safi la kizazi cha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) huku akiwa ni mbora wa wanawake wote ulimwenguni.

Historia yake ni sawa na historia ya utume kwani alizaliwa kabla ya Mtume (s.a.w.w.) kuhama, na akafariki miezi michache baada ya kifo cha Mtume (s.a.w.w.).

Swahili

Somo La Kumi Na Tano: Fatima Az-Zahrau Mama Wa Maimam Watakasifu

Nasaba Yake Tukufu

Hakika kiungo kati ya uimamu na utume ni Fatima binti Muhammad, mama wa Maimam maasumina na mbora wa wanawake wote wa ulimwenguni. Mama yake ni mbora wa wanawake wa kikuraishi, Khadija binti Khuwaylid bin Asad bin Abdul-Uzza bin Quswayy, na yeye ndiye mke wa kwanza wa Mtume (s.a.w.w.) na yeye alitokana na nyumba yenye elimu na sharafu. Hakika kumzaa mtu kama Fatima Az-Zahrah mkweli, mtakasifu na maasumu kunatosha kabisa kuwa utukufu mkubwa kwake.

Swahili

Somo La Kumi Na Nne: Urithi Wa Imam Ali (A.S.)

Falsafa ya utawala na nidhamu yake

Kwanza: Utawala Ni Dharura Ya Kijamii

Uimamu ni mpangilio wa umma.
Lazima watu wawe na kiongozi, awe mwema au mwovu.

Swahili

Somo La Kumi Na Tatu: Urithi Wa Imam Ali (A.S.)

Baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.) hatupati hazina kubwa yenye rutuba iliyokamilika na iliyo maarufu kama hazina aliyoiacha Imam Ali bin Abu Talib (a.s.). Na ya kwanza ni hazina inayojulikana kwa jina la kilele cha fasaha, yaani Nahjul-balaghah. Ya pili ni ijulikanayo kwa jina la hekima bora na makusudio ya maneno, yaani Ghurarul- Hikam wa Durarul-Kalim.

Swahili

Somo La Kumi Na Mbili: Sifa Za Imam Ali (A.S.) Na Mwonekano Wake

Urafiki

Laiti kama si mafuriko makubwa ya urafiki wa kweli na huruma iliy- ojaa na kumwagika ndani ya nafsi yake basi Ali (a.s.) asingechagua urafiki penye uadui. Kwa ajili hiyo wanahabari waaminifu kuanzia wafuasi wake hadi adui zake wamepokea kuwa: Pindi Zubayri na Talha walipong’ang’ania kumpiga vita, wakakataa kumtii huku wakimtuhumu katika tukio mashuhuri la vita vya ngamia (Jamal) Ali (a.s.) aliwaendea akiwa hajajiandaa kwa vita, hana ngao wala silaha huku akiwaonyesha amani aliyodhamiria, kisha akanadi:

Swahili

Somo La Kumi Na Moja: Sifa Za Imam Ali (A.S.) Na Mwonekano Wake

Kuifuata Haki

Shakhsia ya Imam Ali (a.s.) ilikuwa na alama dhahiri ambayo ndio makusanyikio ya sifa zake zote na mazalisho ya ukamilifu wake wote, nayo ni kuifuata haki vyovyote itakavyokuwa na popote itakapokuwepo. Kufuata kwake haki kulipatikana tangu kipindi cha mwanzo cha uhai wake kwa kutii amri za Mwenyezi Mungu na Mtume Wake (s.a.w.w.) bila mipaka.

Swahili