Utangulizi

Waislamu wamegawanyika makundi wawili kuhusu maana ya maneno "Ulul-Amr" yaliyotumika katika Aya ya 59 ya Surat An-Nisa.

Wako wasemao kuwa maana ya maneno haya ni "Watawala kutoka miongoni mwenu" - yaani watawala wa Kiislamu; na hii ndio tafsiri ifuatwayo na Waislamu walio wengi (Masunni).

Wako wengine wasemao kuwa, maana ya maneno hayo ni "Makhalifa (au Maimamu) Ma’asumiin (Watakatifu) Walioteuliwa na Allah kushika mahali pa Mtukufu Mtume [s] baada ya yeye Mtume [s] kuondoka. Hii ndio tafsiri ifuatwayo na Mashia-lthna-ashariyah.

Swahili

Ulawiti Dhambi Kuu

Mojawapo ya madhambi ambayo imechambuliwa kama ndilo dhambi kuu ni ulawiti1 au kuingiliana jinsia moja.

Swahili

(11) Wanavyosema Wapinga Maulidi Na Majibu Yetu

Leo tunaanza kuyajibu yaliyochapishwa na "Wakereketwa wa Sunnah Malindi" kwa jina la "Majibu ya Abdillah Nassir". Makala tunayoyajibu leo ni yale ya "chapa ya kwanza". Sijui kama, baada ya hiyo, wametoa chapa nyengine kwa sababu mimi sijaziona. Kama wamezitoa, basi naomba waniletee kwa anwani yangu iliyomo humu ili niweze kuzishughulikia.

Katika makala yao hayo, walianza kwa kusema: "Tunashindwa kukuelewa tukueke wapi …"

Swahili

(10) Wanavyosema Wapinga Maulidi Na Majibu Yetu

Wiki iliyopita tuliona kwamba wapinga maulidi, wanaposoma vitabu vya maulidi, wakaona kuwa Mtume (s.a.w.w.) amesifiwa kwa neno alilosifiwa Mwenyezi Mungu, au kitendo chake kimetajwa kwa neno ambalo, kwa kawaida, hunasibishwa nalo Mwenyezi Mungu -- wanapoona hayo, moja kwa moja husema ni shirki, kwa sababu hivyo ndivyo wanavyoielewa wao shirki, na hali hivyo sivyo.

Swahili

(9) Wanavyosema Wapinga Maulidi Na Majibu Yetu

Wiki iliyopita tuliyataja maneno ambayo Ahlu-Tawheed wameyatoa katika Barzanji na Burdah ambayo, kwa maoni yao, ni shirki. Tukaahidi kuyajadili maoni hayo leo, baada ya kuieleza shirki ni nini.

Swahili

(8) Wanavyosema Wapinga Maulidi Na Majibu Yetu

Kama tulivyoahidi wiki iliyopita, leo tunaanza kuwajibu Ahlu-Tawheed kwa waliyoyaandika katika makaratasi yao waliyoyapa jina la "Uzushi na Shirk Ndani ya Barzanji na Vitabu Vyengine vya Maulidi".

Swahili

(7) Wanavyosema Wapinga Maulidi Na Majibu Yetu

Wiki iliyopita tulidondoa baadhi ya mambo yanayofanywa maulidini ambayo, ama Qur'ani na / au Hadithi zimeyaamrisha, au zimeyapendekeza. Leo tunaendelea na yaliyobaki:

5. Kutoleana waadhi: Katika Qur'ani Tukufu (Sura 16:125) Mwenyezi Mungu anatuamrisha tulinganiane kwa hikima na mawaidha mema. Na vivyo hivyo ndivyo Bwana Mtume (s.a.w.w.) anavyotuhimiza katika Hadithi zake nyingi.

Jee, maulidini hatutoleani mawaidha na kulinganiana mema? Hayo nayo kama ni bid'a, sunna ni ipi?

Swahili

(6) Wanavyosema Wapinga Maulidi Na Majibu Yetu

Kama tulivyoeleza katika makala yetu ya wiki iliyopita, sio kila kitu kimetajwa kinaga ubaga katika Qur'ani na / au Hadithi. Kuna yaliyotajwa hivyo; kuna na yaliyotajwa kwa jumla, kama maulidi. Lau Waislamu (wanazuoni wao) wangekataa kila jambo ambalo halikutajwa kwa jina katika Qur'ani na / au Hadithi, wangelibaki nyuma kwa karne 14, na wasingekuwa na maendeleo yoyote.

Sasa tuje kwenye maulidi.

Swahili

(5) Wanavyosema Wapinga Maulidi Na Majibu Yetu

Tunaendelea na hujja za wanaopinga maulidi na majibu yetu.

Katika hujja yao ya tano wanasema: Hakuna ushahidi wowote, wa Qur'ani wala Hadithi za Mtume Muhammad (s.a.w.w.), unaothubutisha usawa wa kuyasoma maulidi, sikwambii kuyatilia nguvu.

Swahili

(4) Wanavyosema Wapinga Maulidi Na Majibu Yetu

Tunaendelea na hujja za wanaopinga maulidi na majibu yetu.

Katika hujja yao ya nne wanasema: Kwenye sherehe za maulidi hufanywa baadhi ya mambo ambayo ni ya munkar (yanayochukiza, bali ni haramu kamwe, katika sharia ya Kiislamu).

Swahili