Amirul-Mu'miniina Ali [a] Na Kumuapa Mwenyezi Mungu Kwa Haki Ya Mawalii
Tunaangalia kumuapa Mwenyezi Mungu kama ilivyo katika dua za Mawalii wake watukufu.
Kwa mfano: Amirul-Mu'miniina Imam Ali [a] anasema katika maombi yake baada ya Sala ya usiku:
"Ewe Mwenyezi Mungu mimi ninakuomba kwa heshima ya yule aliyejilinda kwako kutokana na adhabu yako na akazitumainia nguvu zako na akajikinga kwa kivuli chako na akashikamana na kamba yako na hakutegemea ila kwako."1