Amirul-Mu'miniina Ali [a] Na Kumuapa Mwenyezi Mungu Kwa Haki Ya Mawalii

Tunaangalia kumuapa Mwenyezi Mungu kama ilivyo katika dua za Mawalii wake watukufu.

Kwa mfano: Amirul-Mu'miniina Imam Ali [a] anasema katika maombi yake baada ya Sala ya usiku:
"Ewe Mwenyezi Mungu mimi ninakuomba kwa heshima ya yule aliyejilinda kwako kutokana na adhabu yako na akazitumainia nguvu zako na akajikinga kwa kivuli chako na akashikamana na kamba yako na hakutegemea ila kwako."1

Swahili

Kumuapa Mwenyezi Mungu Kwa Haki Ya Mawalii

Miongoni mwa nukta wanazotofautiana Waislamu na Mawahabi ni kwamba, Mawahabi wanadai kuwa, ni haramu kumuapa Mwenyezi Mungu kwa haki ya Mawalii, na pia kuapia kisichokuwa Mwenyezi Mungu.

Wakati mwingine Mawahabi wanaona kuwa viapo hivi viwili ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu katika Ibada. Katika maelezo yafuatayo tutaisherehesha kwa urefu maudhui hii ili kupata hukmu sahihi ya kisheria.

Bila shaka Qur'an inawasifu baadhi ya waja wa Mwenyezi Munga inaposema:

Swahili

Kuitakidi Uwezo Wa Ghaib Wa Mawalii Wa Mwenyezi Mungu

Je, kuitakidi kwamba Mawalii wa Mwenyezi Mungu wanao uwezo wa ghaib ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu?

Bila shaka hakuna wasi wasi kwamba, mtu hawezi kuomba haja yake kwa yeyote yule ila atakapokuwa na uhakika wa uwezo wa huyo amuombaye kuwa atamtimizia haja yake na kutekeleza ombi lake.

Uwezo huu umegawika sehemu mbili:

1. Uwezo wa kimaada unaoonekana kama vile kumuomba maji mtu fulani kisha akakujazia maji hayo kwenye chombo na akakupatia.

Swahili

Dalili Za Mawahabi Za Kuharamisha Kuomba Shafaa

Tumetaja ndani ya mlango uliopita dalili zinazoruhusu kuomba Shafaa, zikiwemo hadithi mbali mbali na aya za Qur'an.

Sasa hivi umefika wakati wa kutaja dalili za Mawahabi ambazo wanadai kwamba zinaharamisha Shafaa, zikiwemo hadithi mbali mbali na aya za Qur'an.

Huu ndiyo ule wakati muafaka wa kutaja zile dalili za Mawahabi ambazo wanadai kwamba zinaharamisha Shafaa na kuzijadili (ili Mwenyezi Mungu aithibitishe haki kwa maneno yake). Mawahabi wametolea ushahidi mambo kadhaa katika kuharamisha Shafaa, nasi tunayataja kama ifuatavyo:

Swahili

Kutaka Uombezi Toka Kwa Mawalii Wa Mwenyezi Mungu

Neno "Shafaa" ni maarufu miongoni mwetu sote, nalo tunalitamka mara nyingi katika ndimi zetu katika nyakati na muhala mnamo husika.

Kwa mfano: Yanapofanyika mazungumzo kumhusu mtu fulani aliyetenda kosa fulani na mahakama imemhukumu kifo au kufungwa au namna nyingine, kisha akatokea mtu akaingilia kati na kumuokoa tokana na hukumu aliyohukumiwa, basi huwa tunasema mtu fulani kamuombea (kamshufaia) fulani.

Swahili

Waislamu Na Kuziomba Msaada Roho Takatifu

Ibnu Taimiyyah na wafuasi wake walifanya pupa kutoa hukmu pale walipopinga wakasema, "Masahaba na Tabi'ina hawakumuomba msaada Mtume [s]."

Swahili

Mawasiliano Na Ulimwengu

Je, inawezekana kuwasiliana na ulimwengu wa kiroho? Jawabu linasema kuwa: Ndiyo bila shaka upo uwezekano huo, nasi tutatoa dalili kwa mujibu wa Qur'an tukufu na pia dalili za kielimu.

Kuthibitika kubakia kwa roho isiyokuwa ndani ya mwili, hakatoshelezi kukubalisha kufaa kuomba msaada kupitia kwenye roho hiyo mpaka uthibiti uwezekano wa kuwepo mawasiliano baina ya roho hiyo na ulimwengu wa duniani.

Ndani ya Qur'an kuna aya nyingi zinathibitisha kwamba, mtu kuwasiliana na ulimwengu wa kiroho ni jambo linalowezekana, isitoshe jambo hili limethibitika kwa vitendo kwa mfano:

Swahili

Kuomba Msaada Kwa Mawalii Wa Mwenyezi Mungu Katika Zama Za Uhai Wao

Bila shaka kuomba kitu chochote katoka kwa Mawalii wa Mwenyezi Mungu kuna namna nyingi, nasi tutazionyesha katika mpango ufuatao:

1. Kumuomba mtu aliye hai atusaidie katika ujenzi wa nyumba au kunywesha maji.

2. Kumuomba mtu aliye hai atuombee kwa Mwenyezi Mungu atusamehe.

Namna hizi mbili zinashirikiana kwa kuwa jambo litakiwalo ni la kawaida kimaumbile, na huyo aombwaye anao uwezo wa kulifanya, lakini namna hizi zinatofautiana kwa kuwa ile ya kwanza imefungamana na mambo ya kidunia, na ile ya pili ina mafungamano na akhera.

Swahili

Mambo Ya Al-Qudhai Al-Misri

Baada ya kuwa nimeyahariri (maelezo yaliyotangulia) na kubainisha ufafanuzi wa ibada niliyaangalia kwa makini maneno ya mmoja wa wachunguzi miongoni mwa wanachuoni wa chuo cha Az-har, yaani Ustadh Sheikh Salamah Al-Qudhai Al-Izami As-Shafii ambaye ndiye Mwandishi wa kitabu kiitwacho "Fur-Qanul Qur'an Baina Sifatil-Khaliq Wa Sifatil-Ak-Waan.

Swahili

Taarifu Kamili Ya Maana Ya Ibada

Bila shaka maana na Maf-humu ya Ibada iko wazi katika lugha ya Kiarabu, na lau tutakwa hatuwezi kuiarifisha "Ibada" kwa Taarifu ya kimantik kwa kutumia neno moja, basi ni kama mbingu na ardhi ambazo zina maana mbili zilizowazi, wakati ambapo wengi katika sisi hawawezi kutoa taarifu kamili kwa kutumia neno moja lakini hali hii haizuwii kujengeka maana ya ardhi na mbingu katika akili zetu tunapoyasikia matamko hayo.

Swahili