Sura Ya Saba
Zipo nasaha nyingi ambazo Mtume alimpa Abu Dharr. Hapa tunadokeza kuhusu chache miongoni mwao. Muhammad Harun Zangipuri ameandika ka mujibu ya mamlaka ya ‘Amali’ ya Shaykh Tusi kwamba Mtume alimwambia Abu Dharr:
“Ewe Abu Dharr! Muabudu Mwenyezi Mungu kama vile unamuona Yeye, na Yeye Anakuona wewe na hata kama humuoni wewe.”
“Tambua kwamba kwanza kabisa ibada Yake ni kumtambua, yaani kuelewa kwamba Yeye ni wa kwanza kabla ya chochote. Yeye hana mshirika. Yeye ni wa Milele hana mwisho.”