Mwokozi Yesu: Muhanga wa Mwisho
Kwa mujibu wa Paulo, mwokozi alikuja katika sura ya Yesu: Mungu alimtuma mwanaye wa pekee duniani ili aje apate mateso na hatimaye afe msalabani ili damu itakayomwagika iwe kafara ya dhambi za wanaadamu, kwa hiyo Yesu ndiye aliyetolewa kafara (mhanga). Paulo alipata fikra hii kutokana na kafara zilizokuwa zikitolewa na Wayahudi kwa Mungu - ambapo maelezo yake yanapatikana katika agano la Kale na akahisi kwamba kafara hizi zilitolewa ili kupata msamaha wa Mungu kutokana na madhambi ya watu.