Mwokozi Yesu: Muhanga wa Mwisho

Kwa mujibu wa Paulo, mwokozi alikuja katika sura ya Yesu: Mungu alimtuma mwanaye wa pekee duniani ili aje apate mateso na hatimaye afe msalabani ili damu itakayomwagika iwe kafara ya dhambi za wanaadamu, kwa hiyo Yesu ndiye aliyetolewa kafara (mhanga). Paulo alipata fikra hii kutokana na kafara zilizokuwa zikitolewa na Wayahudi kwa Mungu - ambapo maelezo yake yanapatikana katika agano la Kale na akahisi kwamba kafara hizi zilitolewa ili kupata msamaha wa Mungu kutokana na madhambi ya watu.

Swahili

Mtazamo wa Uislamu juu ya "Mungu Mmoja"

Wakati ukristo unababaika kueleza maana ya "Mungu mmoja" tatizo hilo halipo katika Uislamu:

"Wamekufuru wale wasemao - Mwenyezi Mungu ni mmoja katika (wale waungu) watatu - (yeye ndiye wa tatu wao). Hali hakuna Mungu ila Mwenyezi Mungu mmoja (tu peke yake). (Qur'an 5:73)

Swahili

Ukristo wa Mwanzo

Tertullian, mwanasheria na kiongozi wa kanisa katika mji wa Carthage, alikuwa ni wa kwanza kutumia neno "utatu mtakatifu" katika karne ya tatu alipotoa nadharia kwamba, Mwana na Roho Mtakatifu ni sehemu za Mungu Mkuu lakini wote ni kitu kimoja (Mungu mmoja).

Swahili

Imani ya Kuamini Kuwepo Kwa Mwenyezi Mungu Mmoja Asiyekuwa na Mshirika (Monotheism)

Kamusi iitwayo "Webster's New World Dictionary" imelitafsiri neno "Monotheism" kuwa ni imani kuwa kuna Mungu Mmoja tu".1 Uyahudi, Ukristo na Uislamu zote zinadai kuwa zinaamini na kufuata imani hii. Imani hii ilihimizwa sana na Nabii Musa katika kifungu katika Biblia kinachoeleweka kama "Shema" au shema ya imani ya kiyahudi:

Swahili

Misingi Na Imani Za Ukristo

Tukizungumza kwa haraka haraka, msingi na imani ya Uungu inasema kwamba Yesu ni mwana Mungu - Neno la Mungu lililofanywa mwili.

Hata hivyo, kama tulivyoona hapo nyuma, Yesu mwenyewe hakuwahi kudai kuwa yeye ni Mungu, Paulo alimpa sifa hii kwa sababu moja kubwa: alitaka kupata wafuasi wengi miongoni mwa Warumi na Wagiriki (watu wa mataifa).

Swahili

Mwanzilishi Halisi Wa Ukristo - Paulo Wa Tarsus

Mmoja wa wanafunzi hawa wa Yesu (Wanazareti) aliyeitwa Stephano alielekeza mahubiri yake mbele zaidi ambapo alitoa mahubiri makali kukemea maovu mbele ya Mahakimu wa kiyahudi walioeleweka kama Sanhedrin. Wakifoka kwa hasira kwa sababu ya maneno yake ya "kishetani", mahakimu waliruka na kumkamata, kisha wakampeleka nje ya mji ambako walimpiga mawe mpaka kufa. Kisa hiki kinapatikana katika "Matendo ya Mitume", sura ya 7, katika Biblia.

Swahili

Kazi Na Ujumbe Wa Yesu

"Maana Mwana wa Mtu alikuja kuwaokoa wale waliopotea". (Mathayo18:11)

"Sikutumwa ila kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo". (Mathayo 15:24)

Yesu pia aliweka wazi ni nini Mwenyezi Mungu alimtaka afanye:

"Mimi sikunena kwa mamlaka yangu mimi mwenyewe, ila Baba aliyenituma ndiye aliyeniamuru niseme nini na niongee nini". (Yoshua12:49)

"Msidhani ya kuwa nimekuja kutengua sheria ya Musa au mafundisho ya Manabii, sikuja kutengua bali kukamilisha". (Mathayo 5:17)

Swahili

Agano Lililovunjika

Akiwa amechoshwa na ibada ya masanamu miongoni mwa watu wake, Nabii Ibrahim aliiacha nchi yake karibu miaka 2000 kabla ya Yesu ili apate uhuru wa kumuabudu Mwenyezi Mungu mmoja.

Ilikuwa vigumu kwake kuiacha nyuma familia yake. Hivyo Mwenyezi Mungu alimbariki kwa kumpa watoto wawili wa kiume. Kisha akamfariji Nabii Ibrahim kwa kumwambia kuwa mtoto wake mdogo, Is-haq atafanya naye Agano la Milele. Is-haq akazaliwa katika nchi ya Kiyahudi ya watu "Wateule" wa Mungu. (Baadaye tunaona ahadi ya Mwenyezi Mungu kwa mtoto mwingine wa Nabii Ibrahim, Ismail).

Swahili

Utangulizi

Uchunguzi wa karibu, katika dini mbili kati ya hizi - Uyahudi na Uislamu - utaonyesha hili kuwa ni kweli: Wote Wayahudi na Waislamu wanamuabudu Mungu mmoja, Muumba wa Mbingu na Ardhi.

Hii dini nyingine, Ukristo, ina mushkeli kidogo, hususan wakati tunapoelezea maana ya imani ya kumuamini Mungu Mmoja asiyekuwa na mshirika tofauti na inavyoaminiwa na Ukristo.

Swahili

Dibaji

Wengi wetu tunaridhika kuishi tu bila udadisi na tunayakubali mambo "kama yalivyo"; tunayapuuza na kuyadharau maswali madogo madogo yanayohitaji kujibiwa na yanayoleta mashaka katika akili zetu, hasa masuala yanayohusiana na dini. Kwa kufanya hivi, ndiyo ni kweli kwamba tunayopuuza, lakini kamwe hatupati utulivu wa akili na amani ndani ya nafsi zetu, kwa sababu daima nafsi zetu zinataka kuujua ukweli na sio kuupuuzia.

Swahili