Tukio La Jamal
Jamal ni ngamia. Inaposemwa Tukio la Ngamia, maana yake yule ngamia aliyempanda Mwana Aisha akaenda nae katika uwanja wa Basra.
Katika mwaka wa thelathini na sita Hijria, Talha na Zubeir walimuomba ruhusa Imam Ali kwenda Makka kwa ajili ya Umra. Walipokuwa njiani wakakutana na Mwana Aisha akawauliza habari za Uthman, wakamwambia kuwa Uthman ameuliwa. Mwana Aisha akasema "Muuweni na'athala hakika amekufuru."
Taz: Tarikh Ibn Athir J.3 Uk. 206
Lisanul Arab J.14 Uk. 193
Assiratul Halabiyya J.2 Uk. 286