Ndoa Ya Mut'a Katika Sunna
Imepokewa kwa Jaabir Bin Abdullah Al'Ansar amesema:-
"Sisi tulikuwa tukifanya Mut'a wakati wa Mtume S.A.W. na wakati wa Abubakar na nusu katika utawala wa Umar, kisha akaikataza Umar."
TAZAMA:
• Fat'hul Bari J. 11 uk. 76
• Umdatul Qary J. 8 uk. 310
• Sharhu Sahihi Muslim J. 8 uk. 233
• Musnadu Ahmad J. 3 uk. 380
• Bidayatul Mujtahid J. 2 uk. 58
• Zadul Maad J. 1 uk. 208 - 209.
Sheikh Muhammad Sharif yeye anasema"ILIKUWAKO" si sawa na "IKO MPAKA LEO" Basi jambo gani lililofanya Shia waamini iko mpaka leo? Ni sababu nne: