Ndoa Ya Mut'a Katika Sunna

Imepokewa kwa Jaabir Bin Abdullah Al'Ansar amesema:-

"Sisi tulikuwa tukifanya Mut'a wakati wa Mtume S.A.W. na wakati wa Abubakar na nusu katika utawala wa Umar, kisha akaikataza Umar."

TAZAMA:

• Fat'hul Bari J. 11 uk. 76

• Umdatul Qary J. 8 uk. 310

• Sharhu Sahihi Muslim J. 8 uk. 233

• Musnadu Ahmad J. 3 uk. 380

• Bidayatul Mujtahid J. 2 uk. 58

• Zadul Maad J. 1 uk. 208 - 209.

Sheikh Muhammad Sharif yeye anasema"ILIKUWAKO" si sawa na "IKO MPAKA LEO" Basi jambo gani lililofanya Shia waamini iko mpaka leo? Ni sababu nne:

Swahili

Ndoa Ya Mut'a Katika Quran

Muenyeezi Mngu amesaema: "Mnaostarehe nao katika wao, (Wanawake) basi wapeni mahari yao yaliolazimishwa" 4:24. Aya hii imeshuka katika ndoa ya Mut'a kama ilivyo atika Tafsiri zifuatazo:-

1. Tafsirut Tabari J. 2 uk. 9

2. Addurrul Manthur J. 2 uk. 140

3. Tafsir Ibnu Kathir J. 1 uk. 486

4. Mukhtasar Tafsir Ibnu Kathir J. 1 uk. 375

5. Tafsirul Qurtubi J. 5 uk. 130

6. Tafsirui Khazin J. 1 uk. 506

7. Tafsirul Kash'shaf J. 1 uk. 519

8. Tafsirul Kabir J. 3 uk. 200

9. Tafsirul Maraghi J. 5 uk. 8

10. Tafsirul Alus J. 5 uk. 5

Swahili

Unayo Majibu Manne

Mifano aliyotoa haiwezi kukubalika katika mahakama yoyote adilifu. Mashahidi watatu wataje miaka mitatu tofauti ya kitendo kimoja?!

Ieleweke kuwa hapo inayohusika si miaka (wakati) peke yake, na mahala vilevile.

Tazama imetajwa, Khaybara na Makka Je! Mashahidi wako wakisema: Waliona ukimkopesha Mombasa shilingi elfu moja, wapili Dar es Salaam, watatu Kampala. Bado hapana Idhtirab??

Swahili

Majibu Yetu

1. Ni wazi hili ni jambo Mukhtalafun fihi kwa hiyo halina Ijamaus Sahaba, basi, huweza kuliharamisha.

2. Kwa nini hakuzitaja hizo riwaya kumi na nane za Imam Ali ili tuzijibu?!

3. Sisi tunasema:- Siyo kweli kuhusu Imam Ali, kama tutakavyoonyesha katika kitabu hiki, na hapo atakapozitaja riwaya nyingine.

Sasa, tutazichambua hoja zake, moja moja, nazo ni hizi:-

Swahili

Uwiano Wa Ndoa Ya Mut'a Na Ya Daima

1. Ndoa ya Mut'a na ya daima, hazithibiti ila kwa kufungamana na matamko mawili: IJABUN na QABUL (Nimekuoza, Nimekubali).

2. Kufungamana kwa ndoa mbili hizi hakupatikani ila kwa moja kati ya matamko matatu haya: ZAWWAJ'TUKA, ANKAH'TU KA, MATTA'ATUKA.

3. Ndoa mbili hizi hupatisha haramu kwa: Nasabu, Ukwe, Kunyonya.

4. Mtoto wa Mut'a ni kama mtoto wa ndoa ya daima, anazo haki zote.

Swahili

Kurithi

a) Mwanamke Ahlulkitabi aliyeolewa na Mwislamu, hawezi kumrithi mumewe.

TAZ: Bidayatul Mujtahid J. 2 uk. 381 Sublus salam J. 3 uk. 954

b) Mwanamke aliyemuua mumewe. Amesema Mtume S.A.W. "Muuwaji hana kitu."

TAZ: Fiqhus Sunna J. 3 uk. 427.

Kwa hiyo majibu yetu hapa ni:-

Ndoa ya Mut'a inatimia bila ya Waiji, wala shahidi, wala chakula, wala kurithiana.

Swahili

Mut'a

Kwanza kabla ya yote lazima tujue Mut'a ni nini.

Sheikh Muhammad Sharif ameeleza hivi "Nikaha ya Mut'a ni:Mtu kukutana na mwanamke akamwambia: Mama! hebu nikuoe kiasi cha dakika kumi". Amuoe kwa dakika kumi, akisha ampe kama ni shilingi kumi an shilingi tano, khalas! mambo yamekwisha. Hiyo ndiyo nikaha ya mut'a, haina haja ya shahidi, haina haja ya Walii, hakuna habari ya chakula, hakuna kurithiana, na muda ukisha, khalas, hakuna nikaha tena mpaka uongezwe (baada ya kuieleza hivyo, akasema) Sallaaaaa La! Si upuuzi huo. (watu wakacheka) Mwisho wa kunukuu.

Swahili

Utangulizi: Mut'a Ndoa Sahihi

Alhamdulillahi, kila sifa njema ni ya Mwenyeezi Mngu, Bwana wa walimwengu. Na Rehma na Amani zimshukie Bwana wetu na Muombezi wetu Muhammad S.A.W., na ziwashukie Aali zake watakatifu, na wanaofuata na kuusimamia uongozi wao mpaka siku ya mwisho.

Ndoa ya Mut'a ni katika mas'ala waliyokhitilafiana Shia na Sunni kutoka mwishomwisho wa utawala wa Khalifa wa pili (Umar bunul Khattab) mpaka leo. Tarehe 17/8/1988 kwa tarehe 3 Muharram 1408 katika ukumbi wa Bilal house, Mombasa, nilizungumza juu ya ndoa ya Mut'a.

Swahili

Sera Za Utawala Baada Ya Mtume

Ukisoma Terikh, na kisha ukafuatilia sera za utawala wa makhalifa watatu, utajua wazi kwamba mabwana hao walizuia kuandikwa Hadithi za Mtume Muhammad (s.a.w.) bali walikataza hata kuzizungumza mbele za watu. Kwa sababu walijua wazi kuwa sera za utawala wao haziendi sambamba na uongozi wa Mtume Muhammad (s.a.w.). Abubakr amekataza kuzungumza chochote juu ya Mtume (s.a.w.) na amesema: Yeyote atakaewauliza mseme: "Kati yetu sisi na nyinyi ni Qur'an, basi, halalisheni halali yake na haramisheni haramu yake".

Taz: Tadh'kiratul hufaadh J. 1 Uk. 3

Swahili

Ahlul Bayt Walio Pamoja Na Qur'an

Imam Ali bin Abi Talib (a.s.) amezaliwa ndani ya Al' Kaaba siku ya Ijumaa, tarehe kumi na tatu Rajab mwaka wa thalathini (mwaka wa ndovu).

Wamekhitilafiana waandishi wa tarikh kujuwa tarehe aliyopigwa dharba Imam Ali, baadhi ya kauli hizo zasema:

Alipigwa dharba tarehe 17 usiku wa kuamkia Ijumaa mwezi wa Ramadhan, akafishwa usiku wa kuamkia Jumapili tarehe 19 Ramadhan.

Alipigiwa dharba tarehe 19 usiku, akafishwa tarehe 21 Ramadhan mwaka 40.

Alipigwa dharba kuamkia tarehe 21, akafishwa tarehe 23 Ramadhani.

Swahili