Mzozo Kati ya Wafuasi wa Madhehebu na Kukufurishana Baadhi Yao Kwa Baadhi

Katika aina ya mzozo baina ya wafuasi wa madhehebu ni kwamba wa Hanbali walikuwa wanachoma moto misikiti ya watu wa Shafi, makhatibu Wakihanafi walikuwa wanawalaani Hanbali na Shafi juu ya mimbari na ilitokea fitina baina ya wa Hanafi na Shafi hata masoko na madrasa zilichomwa moto.1

Swahili

Kauli za Maulamaa Kwa Maimamu

Khatibu Al-Baghdad amepokea kwa Isnad kutoka kwa Wakii amesema: walikutana Sufiyan Thauriy, Shariki, Hasan bin Swaleh na Ibn Abiy Laila; wakamwita Abu Hanifa, akawajia, wakamwambia: "Unasemaje juu ya mtu aliyemuuwa baba yake? Akamuoa mama yake na akanywa pombe akiwa amekaa juu ya kichwa cha baba yake?"

Swahili

Tutamfuata (Tutamqalidi) Nani?

Tukiachilia mbali kauli za maimuamu wanne katika kukataza kufuatwa kwao, tukijaalia kuwa kuna dalili, tutamfuata nani? Je, tumfuate Abu Hanifa au Malik au Shafi au Ahmad? Hakika kilicho bora kimekosekana, na kuchagua kilicho bora bila ya kuwepo kilicho bora ni uharibifu kiakili na kisheria, mfano kama tutamfuata Shafi, hii si ina maana kwamba sisi tumeweka kwa wengine alama ya kuuliza? Na tatizo ni kwamba madhehebu ya Ash’ariy ya kifiqihi ni mahala pa Ikhitilafu, watu wa Hanafiy wanasema ilikuwa ni wa kihanafy, Malik wanasema alikuwa ni wa Malik na shafi kadhalika wanasema ni Shaafiy!

Swahili

Sehemu ya Kwanza Pamoja na Ash’ariah

Kwa nini niwe Asha'riah?

Kwa nini ni wajibu nimfuate Ash'ariy na moja ya madhehebu manne? Je, kuna dalili? Je, kuna Aya? Kuna Hadith?

Tukirejea kwenye Qur'an na Sunna hatupati hata ishara ndogo juu ya jambo hili, anasema Jaadul -haqi Ali Jaadul-haqi- Sheikh wa Azhari: "Hailazimu kauli ya mwenye kusema kuwa kuna ulazima wa kumfuata mmoja wa maimamu, Abu Hanifa, Maaliki, Shaafiy na Ahmad bin Hanbali wakati hakuna dalili juu ya hilo."1

Swahili

Utaratibu Wetu Katika Utafiti

Utaratibu wetu katika utafiti huu ni kulitaka kila kundi lilete hoja yake kutoka katika kitabu na Sunna juu ya usahihi wa madai yake kwa sababu ni wajibu kwa hao watu kuuchukua Uislam wao kwao, utarat- ibu wetu ni Qur'an, anasema Mwenyezi Mungu: "Sema leteni dalili zenu kama nyinyi ni wa kweli”1 na “ambaye mizani ya amali zake njema itakuwa nzito, Basi atakuwa na maisha mazuri."2

Swahili

Katika Zama za Mtume (s.a.w.w)

Maswahaba (r.a) walikuwa wanarejea kwa Mtume (s.a.w.w) katika mambo yanayowatokea, naye alikuwa anawajibu kulingana na sheria ya Mwenyezi Mungu, na sisi tunajua kuwa Mtume (s.a.w.w) asingebaki milele ili watu wamrejee kwa mambo ya kidini na kidunia, alifariki (s.a.w.w) baada ya kutimiza vizuri wajibu wake, na lazima awepo atakaye bainisha vizuri sheria za Mwenyezi Mungu, ubainifu ulio kamili na sahihi ambapo Mwislamu atapata matumaini kwayo na kwamba kauli yake hii ndiyo makusudio ya sheria.

Swahili

Kuondoa Kikwazo

Inaonyesha kuna kikwazo mbele yetu na ni lazima tukiondoe kabla ya kuingia ndani ya maudhui kwani mtu anaweza kusema: "Hakika kutoa maoni katika maudhui kama haya, humo kuna kupinga fikra za watu wengine na viongozi wa madhehebu.

Swahili

Itikadi na Athari ya Mazingira

Hakika mazingira na nyakati mara nyingi zimekuwa na athari kubwa katika kupanga fikra ya binadamu na mwelekeo wake, ambapo urithi wa kimazingira unakuwa kadiri muda unavyopita pamoja na kuzoeleka, kimaneno na kitabia unakuwa ni ukweli thabiti ambao hawezi kuuepuka; mwanadamu akitokewa na jambo linalopinga itikadi zake, athari za kifikra za jamii yake ambazo zimeshatawala katika mishipa yake zinajitokeza bila kuhisi na kusimama kidete kupinga kila anayezikhalifu, lakini Mwislamu ambaye ni mtu adhim, dini inamlazimisha kukaribisha fikra za wengine na kuzijadili kwa uhuru na kwa maudhui.

Swahili

Maudhui Haya ni ya Nini?

Mtume (s.a.w.w) alitupa habari kwamba umma wake utagawanyika makundi sabni na tatu, yote yataingia motoni isipokuwa moja litaingia peponi.1 Na leo tunaona kwamba waislamu wako makundi mengi na kila moja linadai liko katika haki, na nimeona jambo hili ni muhimu sana na kwayo imesimama hatima ya waislamu, hivyo ni muhimu sana kwa kila mwislamu anayetaraji nusura siku ya Qiyama lazima ajitahidi

Swahili

Mwanzo wa Safari

Mbingu inaiangazia ardhi, na kuangaza njia zake zinazopitika, mwanadamu hajui lugha yake, na wakati mwingine hufanya njama bila ya kuelewa ili kuzuia mionzi yake pamoja na yote hayo halichoki, mikono yake inabaki imekunjuka ili huenda ataongoka yule atakayeikamata na kupata uongofu.

Jua linaelea angani na udanganyifu umemeza sehemu kubwa miongoni mwa nuru yake katika wakati huu, na katika moja ya njia za kijiji changu kilichojawa na ugeni, ilinijia taufiq iliyokuwa imejificha katika maneno ya rafiki yangu ambaye amekuwa rafiki yangu tangu utotoni.

Swahili