Kisa Cha Kujitolea H. Ali Roho Yake, Usiku Wa Kuhama Mtume Makka

Ma'mun: Hebu kidogo nieleze kuwa yule mwenzi ambaye alikuwa na Mtume (s.a.w.w) katika pango, au bwana yule ambaye alijitolea roho yake na kumhifadhi Mtume, na akalala mahala pa Mtume hadi akaweza kuhama; bora yupi?

Swahili

Maelezo Ya Majadiliano Kati Ya Ma'mun Na Wanachuoni Kuhusu Sifa Za Ali Bin Abi Talib

Is-haq bin Ibrahim bin Ismail bin Hamad bin Zayd amesimulia kwamba siku moja Yahya bin Aktham Qadhil ­Qudhat (Kadhi mkubwa) alinitumizia mimi na baadhi ya sahibu zangu katika wanachuoni, kusema, "Kuwa Ameerul Mumineen ameniamrisha kesho alfajiri niwachukue watu arobaini, wote wawe Faqeeh wenye elimu ya kutosha, wanachuoni wa Fiqhi wawe na uwezo wa kufahamu wanachoambiwa na kujibu vizuri", basi wataje hao ambao unadhani kama watafaa kwa yale anayoyataka Ameerul Mumineen." Tukamtajia idadi maalum na yeye pia akawataja idadi maalum, hata wakatimia arobaini (40) kiasi alichotaka, na wakaandikwa

Swahili

Majadiliano Kati ya Ma'mun na Wanachuoni Kuhusu Sifa za Ali Bin Abi Talib (a.s)

Dibaji Ya Toleo La Kwanza

Kitabu hiki ni tafsiri ya mazungumzo kati ya Khalifa mashuhuri wa Kiislamu aitwaye Ma'mun Ar-Rashid na wanachuoni arobaini wa Ki-islamu wenye elimu ya juu kabisa zama hizo. Jambo waliojadiliana ni ubora wa Seyyidna Ali bin Abi Talib (a.s) juu ya Masahaba wengine wa Mtume Mtukufu (s.a.w.w).

Swahili

Mwisho

Ni bora kwa waislamu waadilifu kuacha ambayo wameyaandika wapinzani wa Shi’a dhidi yao na waanze wenyewe kwa akili zao utafiti juu ya ukweli. Vitabu vya Shi’a vimeenea kila sehemu na kuna uwezekano wa kuwasiliana na taasisi zao na maulamaa wao.

Si dai katika utafiti huu kwamba mimi nimefikisha Ushi’a wote kwa ukamilifu wake kwa wasomaji, utafiti ni mpana katika jambo hili na muhtasari huu hauwezi ukaubeba wote.

Na ifuatayo ni baadhi ya orodha ya vitabu tunaiweka mbele ya watafiti kwa anayetaka ziada ya utafiti katika maudhui haya:-

Swahili

Raja'ah

Raja'ah: kwa Shi’a ina maana kwamba Mwenyezi Mungu atawarejesha katika siku za mwisho wa Dunia watu miongoni mwa wafu katika wale waliobobea katika imani na wale waliobobea katika ukafiri, Mwenyezi Mungu atalipiza kisasi hawa kwa wale.

Na itikadi hii sio muhimu sana katika madhehebu ya Shi’a na haina uzito kwa Shi’a ni kama vile imani juu ya Dajali na mambo mengine, amesema Kaashiful-Ghitrwaa.

Swahili

Al - Badau

Al-badau ni tuhuma miongoni mwa tuhuma ambazo wapinzani wa Shi’a wanaieneza dhidi yao kwa msukumo wa kimadhehebu bila ya kutazama kwa kina katika kusoma hoja ambazo Shi’a wamefahamu kutoka kwayo. Bali wapinzani wa Shi’a wanazidi kuelekeza tuhuma na kuwalaumu kwa sababu yake hadi Al-badau imekuwa ni moja ya tofauti za kimadhehebu ambazo zimetenganisha Shi’a na wasio kuwa wao.1

Swahili

Turbah ya Husein

Ma-Shi’a wanatumia turbah (kipande cha udongo) iliyotengenezwa kwa udongo kusujudia juu yake, na baadhi ya waandishi wamepata fursa ya kushambulia Shi’a, na katika kufafanua jambo hilo tunasema: "Hakika kanuni katika madhehebu ya Ahlul-Bait ni kwamba haijuzu kusujudu isipokuwa kwenye ardhi au kilicho ota ardhini ukiondoa vinavyoliwa na kuvaliwa.

Swahili

Taqiya

Inawezekana kufahamu kimakosa taqiya ndiko ambako kume sababisha baadhi kuwashambulia Shi’a, hakika Shi’a hawakujificha vitabu vyao vya rejea ambavyo humo wamechukua itikadi yao vime-enea, na wao wamevichapisha na kuvisambaza kwa watu wa madhehebu mbalimbali, taqiya sio udanganyifu, hadaa na unafiki kama wanavyoita baadhi lakini nikuficha itikadi katika baadhi ya nyakati kwa kuzuia adha kwa wengine.

Swahili

Shutuma Kuhusu Imamiya

Hakika walioandika kuhusu Shi’a walikwepa ukweli pale waliporejea vitabu vya wapinzani na wakanukuu kutoka kwao bila ya kuhakiki wala kutazama.

Swahili

Utaratibu Wa Ahlul-Bait (a.s)

Utaratibu wa Ahlul-Bait (a.s) umesimama juu ya kushikamana na Kitabu na Sunna na kuepukana kutoka na kufuata qiyasi na rai ……. Imamu Ali (a.s) alishaandika Sunna Wakati wa Mtume (s.a.w.w) na kitabu chake kimejulikana kwa jina "Aswahifah" na Maimamu wa Ahlul-Bait wanaachiana kitabu hicho na wamekitegemea kwa mapokezi kutoka kwa Mtume (s.a.w.w). Na hizi ni baadhi ya kauli za maimamu ili tujue mshikamano wa manhaji yao iliyo madhubuti.

Swahili