Utangulizi wa Chapa ya Pili

Shukrani zote ni za Mola wa viumbe, amani na rehema za Mwenyezi Mungu zimshukie Muhammad na Ahali zake wema watoharifu.

Giza halijaacha kueneza nguvu zake za upofu ili kuzuia mwanga wa nuru tukufu ya Mwenyezi Mungu, na linajaribu kuziba kila njia wanayoifikiria wapenzi watukufu katika kuingia humo, lakini jua linatoa mwanga wake juu ya ardhi bila ya kujali mkusanyiko wa mawingu yenye giza nene, ambayo yameafikiana kuzuia nuru yake.

Swahili

Utangulizi wa Chapa ya Kwanza

Shukrani zote ni za Mwenyezi Mungu ambaye aliwatuma Mitume wake kwa ubainifu na akateremsha pamoja nao vitabu na mizani hali ya kuwa ni rehema na uongofu kwa watu. Rehema za Mwenyezi Mungu zimshukie mteule Muhammad na Ahali zake waongofu rehema ya daima isiyo na mipaka, idadi wala kikomo.

Swahili

Dibaji

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu

Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w): "Nimewaacha katika njia iliyowazi, usiku wake ni kama mchana wake hatotoka humo baada yangu isipokuwa mwenye kuangamia.'' (Musnad Ahmad J:4 uk:126).

Swahili

Neno la Mchapishaji

Kitabu kilichoko mikononi mwako, ni tarjuma ya kitabu cha Kiingereza, kwa jina la "Ikramataniy Al-Samai" kilichoandikwa na Mwanachuoni mkubwa, mwanahistoria na mtafiti Mar'wan Khaliyfat.

Kitabu hiki kama kile cha "Ukweli wa Ushi'a" ni utafiti na mjadala juu ya hitilafu baina ya Shi'a na Sunni. Mwandishi ametumia njia nyepesi sana ya kumuwezesha kila msomaji wa kiwango chochote kuweza kuelewa mada zote alizozijadili katika kitabu hiki.

Swahili

Wasiya Kwa Mwanamke Mu’umin

Katika historia yetu adhimu, mwanamke ana sehemu kubwa na ya kijasiri, ambayo mara nyingine yamu­onyesha akiwa kwenye uwanja wa mapambano, na wakati mwingine kwenye medani ya kupambana na ubatili, kuanzia bibi Maryam, bibi Khadija, bibi Fatima, bibi Zainab, Ummu Ammar na wengineo.

Swahili

Kupanga Uzazi… Kwa Nini?

Mnamo mwaka 1965 huko Bombay, India, kulianzi­shwa shirikisho la kimataifa la kupanga uzazi (Fa­mily Planning), ambalo baadhi ya nchi za kiislamu zilijiunga. Sababu walizozitoa za kuanzishwa kwa shirikisho hilo ni kama ifuatayo.

Tatizo la makazi:
Ongezelo kubwa la watu duniani kila mwaka halilingani na uzalishaji mdogo wa chakula duniani, kwa hivyo ni lazima kupunguza ongezeko hilo ili kujiepusha na njaa.

Umuhimu wa malezi ya watoto:
Familia inayoweza kulea watoto watano mathalan katika hali ya kawaida, itaweza kulea watoto wawili kwa vizuri zaidi.

Swahili

Kuiga: Maafa ya Ulaya Mashariki

Watu wa Ulaya mashariki walipojitenga na dini tu, hadhi yao ikaporomoka wakawa ni wenye kuiga tu. Wengine nao walipofika mwezini, vijana wetu nao wakavutiwa sana na hilo wakasoma magazeti yao ili wapate ramani iliyowafikisha huko mwezini lakini hawakuipata, ila tu waliambulia bimbiriza – mavi, habari za vijana wa Pop Music na fikra ya uhuru, wao wakadhani mambo haya ndiyo ramani ya kufika mwezini. Wakaacha kila kitu. Wakavaa mavazi ya kike! Jee! hii si aibu?

Hapana, maadam Waamerika wanafanya basi si aibu, si wao wamefika mwezini? Hayo ndiyo maneno yao.

Swahili

Barua Ya Haraka Kwa Msichana Wa Karne Ya Ishirini Na Moja

Kwako msichana wa karne ya ishirini na moja.

Wale wanaopigania uhuru hawakupiganii wewe, ati mwanamume fulani apigania uhuru wako kama unavyofahamu, sivyo, bali hao wenye njaa wanapi­gana wapate uhuru kwenye mwili wako wakuvutia, au ati mwanamke fulani atake uwe huru kwa sababu yeye yuhuru, la hasha, anachotaka ni kukuingiza wewe uwe pamoja naye katika pepo hiyo na mapo­chopocho, yeye anapotea na ataka wewe pia uanguke kwenye shimo la maovu kama yeye ili umuondolee hisia zake za kujiona yuko peke yake katika maovu hayo.

Swahili

Kuhusu Mwanamke

Hao… wanataka kutokomeza familia…

Familia inapokuwa imejengeka kwa misingi ili­yowekwa na Uislamu, basi inakuwa imara na yenye mshikamano na hivyo ni muhali kuisambaratisha. Na familia inaposhikana kiasi hiki watoto hukua katika mazingira ya kidini wakiwa na pambo tukufu; na hii inafanya jamii kuwa ni yenye kuhifadhika na upotofu kusambaratika na kufanywa watumwa, na sote tuna­jua kwamba kusambaratika ndiyo kipimo cha nguvu ya ukoloni. Free Mason, ili kufikia hilo wanasema:

Swahili

Ratiba Kwa Vijana

Imam Ali (a.s) amesema: “Waangalieni sana vijana, na hasa wale wadogo…”

Amesema pia: “Moyo wa kijana mdogo ni kama ardhi ambayo haijalimwa, kila utakachokipanda kitapokewa (kitamea).”

Kwa hivyo kuwashughulikia wavulana na wasichana ni muhimu sana kuliko kuwashughulikia watu wazima, haifai kuwatelekeza kwa sababu ya umri wao mdogo, huenda ikawa msichana aliyeshikamana na dini wakati wa udogo wake akawa ana nafasi kubwa na akaweza kutoa huduma kubwa sana kwenye njia ya Mwenyezi Mungu.

Swahili