Kufariki Kwake

Baada ya maisha yenye shughuli namna hiyo kuna uwezekano wa kupatikana wakati wo wote ule kwa ajili ya fitina za kisiasa au lo lote lile lifananalo na hilo? Lakini kuongezeka kwa mvuto wake kwa watu katika mambo ya Kiroho na kuwa kwake chanzo cha Elimu ya Kidini vilikua ndiyo sababu kubwa ya watawala kutaka kuyaondoa maisha yake.

Swahili

Umaarufu Wake Wa Kielimu

Ingawa aliishi miaka ishirini na nane tu, aliiua kiu ya kisomo ya wanachuoni wengi wa wakati ule na pia aliweza kupambana vya kutosha na mafalsafa wa wakati huo ambao walikuwa wakieneza mambo yaliyokuwa kinyume cha mafundisho ya dini.

Swahili

Maadili Yake

Maisha yake yalikuwa ni yale ya wenzake wa Ukoo wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Alikuwa wa pekee katika upole ustahmilivu, ukarimu, uvumilivu, huruma na Kumuabudu Mungu kwake kulifanyika kiasi ambacho, hata wakati alipokuwa kafungwa katika kizuizi kikali sana kila Mu'tamad alipoulizia habari zake, aliambiwa kuwa Imamu alikuwa aki funga mchana na usiku kucha akisali na alikuwa hasemi neno ila maneno ya ibada tu.

Ingawaje Imamu (a.s.) alikuwa na uhuru mdogo sana hata hivyo ilipowezekana watu walikwenda kumwona na kutoa hamu yao ya kujifunza na walirudi wakiwa wametosheka kabisa.

Swahili

Kuteuliwa Kwa Wajumbe

Maimamu wa Ukoo wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wakati wote walifanya kazi zao wakiwa Maimamu katika hali zote. Imamu Hasan Askari (a.s.) alikuwa akiishi katika vizuizi vya namna nyingi sana kwamba ilikuwa vigumu kwa wenye kupenda kujifunza kutoka kwa Imamu kuweza kuonana naye. Hivyo Imamu aliwateua watu wenye kuaminika kutokana na uaminifu wao kuelewa kwao na elimu yao. Wajumbe hawa waliwaongoza watu kwa kadiri ya uwezo wao na kama palitokea tatizo lililokuwa zaidi ya uwezo wao basi walingojea mpaka wapate nafasi ya kumuona Imamu ili awape majibu na wao wawape watu.

Swahili

Wafalme Na Maongozi Yao Ya Serikali

Mu'tazz Billah Abbasi alikuwa Mfalme wakati Imamu Hasan Askari (a.s.) alipopata Uimamu. Baada ya Mu'tazz kupinduliwa, Muhtadi alitawala kwa muda wa miezi kumi na moja na siku chache naye alirithiwa na Mu'tamad. Hakuna hata mmoja wa hao Wafalme aliyemwacha Imamu (a.s.) akae kwa amani. lngawaje Serikali ya ukoo wa Bani Abbas ilikuwa katika machafuko, licha ya matatizo hayo yote wote waliona afadhali kumwacha Imamu (a.s.) abaki humo jela.

Swahili

Utangulizi

Uislamu haukuwa mkusanyo wa mafundisho ya kanuni tu. Uliletwa ili uwe kitu cha kutumika kutatulia matatizo ambayo yanawatokea watu katika maisha yao ya kila siku. Uislamu hauweki mawazo ya kielimu tu ambayo hayana kiini cha maisha halisi, bali hutoa mifano bora ya maisha ya Uchamungu na maisha maizuri.

Swahili

Imamu Katika Qur'an Na Hadithi

Mwenyezi Mungu anasema:

(Ewe mwanadamu! Ikumbuke) siku tutakapowaita kila watu pamoja na Imamu wao; basi atakayepewa kitabu (chake cha Amali) kwa mkono wa kulia, hao watavisoma vitabu vyao (kwa furaha); ... (Bani Isra'il, 17:71)

Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema:

Yeyote yule afaye pasi na kumjua Imamu wa zama zake, atakuwa kafa kifo cha ujinga".

Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema:

Swahili

Idhaa Ya Sauti Ya Ujerumani

Tarehe 18/9/1989, katika majira ya saa moja kasorobo asubuhi. Sauti ya Ujerumani ilitangaza kuwa "Katika nchi ya Morocco, ndoa ya Mut'a imeshika nguvu sana. Vijana wa kiume na wakike wanaowana Mut'a kwa idadi kubwa, na inasemekana kuwa Masaudi wengi wanakwenda Morocco kwa ajill ya kuowa Mut'a. Mwanamke wa Morocco hujulikana kuwa ameolewa Mut'a kwa kuonekana mapambo ya dhahabu aliyonayo ambayo huyapata kwa Masaudi."

Swahili

Aya Ya Mut'a Imefutwa?

Wanasema:- "Aya isemayo: Na ambao kwa tupu zao ni wenye kujilinda, isipokuwa kwa wake zao au kwa (wanawake) wale iliyowamiliki mikono yao ya kuume, basi hakika hao ndio wasiolaumiwa. Lakini anaetaka kinyume cha haya basi hao ndio warukao mipaka" 23: 5-7. Aya hizi zimeiondoa Mut'a. Jawabu: Aya hizi haziwezi kuiondoa ndoa ya Mut'a kwa sababu, Aya hizi zimeshuka Makka, na Aya ya Muta imeshuka Madina. Kwa mujibu wa misingi va Nasikh na Mansukh dai hili limeanguka, litupe nje.

Swahili

Majibu Yetu

1. Riwaya hiyo ni ya Said bin Jubeir, ambae alikuwa akifanya Mut'a Makka na Ibnu Abbas pamoja na wafuasi wake walikuwa wakiiona Mut'a kuwani halali.

TAZAMA: Al'Musannaf J. 7 uk. 496

Tafsirul Qurtubi J.5 uk. 133

Al'Mughuniya Ibnu Quddama J. 7 uk. 571

2. Riwaya hiyo ni nyonge sana.

TAZAMA: Tahdhibut Tahdhibi J. 2 uk. 198.

3. Riwaya hiyo ndani yake mna Hajjaji bin Artat:-

"Amesema Ibnu Abdil Hakami, nimemsikia Shafii akisema:

Swahili