Aya 36 – 40: Nizifikie Njia
Maana
Na Firauni akasema: Ewe Hamana! Nijengee mnara ili nipate kuzifikia njia. Njia za mbinguni ili nikamwone Mungu wa Musa. Na kwa hakika mimi bila ya shaka namjua kuwa ni mwongo tu.
Firauni alimtaka waziri wake Hamana amjengee mnara mrefu ili apande mbinguni kwenda kumtafuta Mungu wa Musa. Alifanya hivi akiwa anajua kabisa kwamba yeye hawezi kufanya hivyo, lakini vile vile anajua kuwa katika anaowatawala kuna wenye akili fupi wasiokwa na mwamko, watakaomsadiki atakayosema. Kwani kauli yake hii sio kubwa zaidi ya kusema: Mimi ndie Mola wenu mkuuu; na asingejasiri kusema hivyo lau sikuweko watakaomwambia: ndio, wewe ndiye Mola mkuu.
Hivi sasa tukiwa katika karne ya ishirini, karne ya maendeleo hadi mtu kufika mwezini, lakini bado Dalai Lama anapata wanaomwambia: Wewe ni Mungu, na Agha Khan naye anapata wanaomwambia; Wewe ni nusu mungu. “Kila mahali kuna Al-kaaba na imam”
Na hivi ndivyo Firauni alivyopambiwa ubaya wa vitendo vyake, na akazuiliwa njia.
Mambo mawili yanampambia mtu matendo yake mabaya: Kufuata matamanio na kuendelea na ujinga. Matamanio yalimpambia Firauni kudai ungu na ujinga ukawapambia wanaomtii.
Na vitimbi vya Firauni havikuwa ila katika kuangamia tu; yaani katika hasara.
Kila aliyejaribu na atakayejaribu kuwahadaa watu na kuwafanyia vitimbi, atakuwa katika hasara; hata kama atakuwa na utawala wa Firauni na mali ya Qaruni.
Na yule ambaye aliamini alisema: Enyi watu wangu! Nifuateni, nitawaongoza njia ya uongofu.
Mumin aliwahadharisha watu wake mara ya kwanza na ya pili. Na hii sasa ni mara ya tatu anawahimiza wakubali nasaha zake, kwa sababu anataka kuwaokoa na wapate kheri. Lakini wengineo wanawaongoza kwenye shari na maangamizi.
Enyi watu wangu! Hakika maisha haya ya dunia ni starehe tu, na hakika Akhera ndiyo nyumba ya daima.
Starehe za dunia zitakwisha tu, hilo halina shaka, lakini maisha ya Akhera yatabakia daima. Basi ni maisha gani kati ya haya mawili yanayofaa kuyafanyia kazi? Katika Nahjul-balagha, imesemwa: “Anafanya nini na dunia aliyeumbiwa Akhera? Na anafanya nini na mali ambaye muda mchache atanyang’anywa na kubakia athari yake mbaya na hisabu yake?” Vile vile imesemwa: “Uchungu wa dunia ni tamu ya Akhera na tamu ya Akhera ni uchungu ya dunia/”
Mwenye kutenda uovu hatalipwa ila sawa na huo, na mwenye kutenda wema, akiwa mwanamume au mwanamke, naye ni Muumini, basi hao wataingia Peponi, waruzukiwe humo bila ya hisabu.
Mwenyezi Mungu ni mwadilifu mkarimu. Uadilifu wake unajitokeza kati- ka adhabu ya muovu. Hiyo mbele ya Mwenyezi Mungu inalingana sawa na malipo. Na hupunguza adhabu kwa huruma zake. Ama mwema huzidishiwa ziada nyingi bila ya hisabu, awe mwanamume au mwanamke. Pepo ni malipo tosha kabisa.
Aya inafahamisha wazi kuwa Pepo ni wakf hususi wa mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, kwa imani isiyokuwa na shaka. Ama yule mwenye kufanya kheri kwa ajili ya kheri tu na huku anamkufuru Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, malipo yake yatakuwa sio Peponi, kwa sababu Pepo si ya makafiri. Tazama Juz. Juz. 4 (3:176 – 178), kifungu: ‘Kafiri na amali njema.’
Kuna mapokezi yanayosema kuwa Mtume (s.a.w.) amesema: “Hakufanya wema mwislamu au kafiri ila Mwenyezi Mungu humlipa.” Akaulizwa: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni yapi malipo ya kafiri? Akasema: mali, watoto, afya nk. Akaulizwa: malipo yake akhera yatakuwa nini? Akasema: Ataadhibiwa adhabu ya chini”
وَيَا قَوْمِ مَا لِي أَدْعُوكُمْ إِلَى النَّجَاةِ وَتَدْعُونَنِي إِلَى النَّارِ {41}
تَدْعُونَنِي لِأَكْفُرَ بِاللَّهِ وَأُشْرِكَ بِهِ مَا لَيْسَ لِي بِهِ عِلْمٌ وَأَنَا أَدْعُوكُمْ إِلَى الْعَزِيزِ الْغَفَّارِ {42}
لَا جَرَمَ أَنَّمَا تَدْعُونَنِي إِلَيْهِ لَيْسَ لَهُ دَعْوَةٌ فِي الدُّنْيَا وَلَا فِي الْآخِرَةِ وَأَنَّ مَرَدَّنَا إِلَى اللَّهِ وَأَنَّ الْمُسْرِفِينَ هُمْ أَصْحَابُ النَّارِ {43}
فَسَتَذْكُرُونَ مَا أَقُولُ لَكُمْ ۚ وَأُفَوِّضُ أَمْرِي إِلَى اللَّهِ ۚ إِنَّ اللَّهَ بَصِيرٌ بِالْعِبَادِ {44}
فَوَقَاهُ اللَّهُ سَيِّئَاتِ مَا مَكَرُوا ۖ وَحَاقَ بِآلِ فِرْعَوْنَ سُوءُ الْعَذَابِ {45}
النَّارُ يُعْرَضُونَ عَلَيْهَا غُدُوًّا وَعَشِيًّا ۖ وَيَوْمَ تَقُومُ السَّاعَةُ أَدْخِلُوا آلَ فِرْعَوْنَ أَشَدَّ الْعَذَابِ {46}