Sema, Tosha Yangu Ni Mwenyezi Mungu Aya 38 – 45
Maana
Na ukiwauliza: Ni nani aliyeziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Mwenyezi Mungu.
Jawabu lao hili linatokana na ufahamu wa kimaumbile aliowaumbia watu Mwenyezi Mungu. Kwa sababu hakuna tafsiri ya kupatikana ulimwengu isipokuwa kuweko Mwenyezi Mungu. Lakini walahidi wanasema: “Sisi hatuamini isipokuwa kwa kujaribu.” Ama maumbile hayo ni maneno ya upuzi. Nasi kwa upande wetu tunawauliza: ikiwa hamuamini isipokuwa majaribio, basi tuonyesheni majaribio yaliyowafahamisha kuwa hakuna Mungu.
Sisi hatuna shaka kuwa mwenye kupinga maumbile haya au kupinga mantiki yake, ndio ameupinga ubinadamu na kupinga yaliyo na thamani zaidi ndani ya binadamu; ukiwemo utashi na uwezo.
Umetangulia mfano wake katika Juz. 21 (29:66) na (31:25).
Sema: Je! Mnawaonaje wale mnaowaomba badala ya Mwenyezi Mungu, ikiwa Mwenyezi Mungu akitaka kunidhuru, wao wanaweza kuniondolea dhara yake? Au akitaka kunirehemu, je, wao wanaweza kuzuia rehema yake?
Washirikina walimtishia Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa masanamu, ndio Mwenyezi Mungu akamwamrisha mtume wake awaambie kuwa masanamu yana uwezo gani kwangu na kwa mwengine? Je, yanaweza kunikinga ikiwa Mwenyezi Mungu anataka kunidhuru? Au yanaweza kuzuia heri anazonitakia Mwenyezi Mungu? Hapana! Masanamu hayawezi kujikinga hata hayo yenyewe ikiwa binadamu anataka kuyavunja kwa shoka au kuyakanyaga kwa kiatu.
Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (6:17) na Juz. 11 (10:107).
Sema: Tosha yangu ni Mwenyezi Mungu. Kwake wategemee wanaotegemea.
Ewe Muhammad! Mwambie anayekadhibisha risala yako kuwa mimi nataka msaada kwa Mwenyezi Mungu na kumtaka mwongozo; naye kwangu ni tosha kabisa! Na yeyote mwenye dhiki basi akimbilie kwake. Yeye ana tosha kuwa walii na msaidizi.
Sema: Enyi watu wangu! Fanyeni muwezavyo, mimi pia nafanya. Basi punde mtajua Ni nani itakayemfikia adhabu ya kumhizi, na itakayemshukia adhabu ya kuendelea.
Yaani kila mtu abaki kama alivyo, kisha tungoje mwisho utakuwaje. Bila shaka itakuwa ni hasara na moto kwenu nyinyi na baraka na neema kwetu sisi.
Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (6:104) na Juz. 11 (10:93).
Hakika Sisi tumekuteremshia Kitabu kwa ajili ya watu wote kwa haki.
Basi fikisha bishara na maonyo, kwa niaba ya Mola wako, kwa kutumia Aya zake; wala usimwachie yoyote udhuru.
Basi mwenye kuongoka ni kwa nafsi yake, na mwenye kupotoka bila ya shaka amepotoka kwa nafsi yake. Na wewe si mlinzi juu yao.
Kila mtu ana majukumu yake na hisabu yake kwa muumba wake, wewe huna majukumu yoyote kwake baada ya kumfikishia na kumpa nasaha.
Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (6:104) na Juz. 11 (10:108).
Mwenyezi Mungu huzipokea roho zinapokufa.
Wanaoamini maada wanasema: Mtu ni huu mwili tu, wala hakuna kitu kingine nyuma yake. Tazama kifungu ‘Wanaoamini maada na maisha baada ya mauti’ katika Juz. 13 (13:5-7). Na ‘Pamoja na wanaoamini maada’ katika Juz. 14 (16:78-83).
Waumini wanasema: Mtu ni mwili na roho, na kwamba roho ndiyo inayouendesha mwili na kuupangilia kwa amri ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Mauti ni kukatika mfungamano wa roho na mwili na roho kwenda kwa Mola wake: “Ewe nafsi iliyotua! Rejea kwa Mola wako hali ya kuwa uradhi mwenye kuridhiwa” (89:27-28).
Na hii ndio maana ya kuwa ‘Mwenyezi Mungu huzipokea roho zinapoku- fa,’ ni kuwa anazishika wakati wa kufa miili.
Na zile zisizokufa wakati wa kulala kwake.
Usingizi ni aina ya mauti au ni mauti kimajazi. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:
وَهُوَ الَّذِي يَتَوَفَّاكُمْ بِاللَّيْلِ {60}
Mwenye Majmaul-bayan anasema: “Inayokufa wakati wa kulala ni nafsi ya upambanuzi na akili ambayo inafarikiana na mwenye kulala, kwa hiyo hawi na akili. Ama ile inayokufa wakati wa mauti ni nafsi ya uhai ambayo inaondoka na pumzi na mwenye kulala huwa anapumua. Kwa hiyo tofauti baina ya kushikwa usingizini na kwisha kwenye mauti ni kuwa usingizi ni kutokuwa macho na mauti ni kutokuwa hai. Na kushikwa usingizini roho inakuwa mwilini na kushikwa kwenye mauti ni roho kuondoka mwilini.”
Huzishika zilizohukumiwa kufa, na huzirudisha nyengine mpaka ufike wakati uliowekwa. Hakika katika hayo bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanaofikiri.
Mwenyezi Mungu kuzishika roho wakati wa kufa mwili na wakati wa kulala. Zile zilizohukumiwa kufa zinabaki kwake na zile nyingine anaziachia zirudi mpaka muda maalum.
Umar bin Al-Khattab alisema: “Ajabu ni kuwa mtu anaota ndoto inakuwa kama kuchukua kwa mkono na anaota ndoto nyingine, lakini haiwi kitu.” Imam Ali bin Abi Twalib akamwambia: “Hakika Mwenyezi Mungu anazifisha nafsi zote. Ile unayoiona iko mbele yake basi ni ya ukweli na unayoiona baada ya kuiachia basi ni ya uwongo.” Akastaajabu Umar kutokana na kauli ya Imam.
Haya ameyanukuu Sheikh Al-Maraghi katika tafsiri yake kutoka kwa Abi Hatim na Ibn Mardawayh.
Au ndio wamejifanyia waombezi badala ya Mwenyezi Mungu? Sema: Ingawa hawana mamlaka juu ya kitu chochote, wala hawatambui?
Masanamu hayatambui kitu, wala hayawezi kujikinga na madhara, lakini pamoja na hayo washirikina wanawatarajia wawaombee mbele ya Mwenyezi Mungu. Hivi ndivyo wanavyofanya wajinga. Muombezi bora zaidi kwa Mwenyezi Mungu kwa wale wenye madhambi ni toba na kurejea kwa Mwenyezi Mungu.
Sema: Uombezi wote uko kwa Mwenyezi Mungu.
Yaani hakuna yoyote anayemiliki uombezi wowote isipokuwa yule aliyemilikishwa na Mwenyezi Mungu:
قُلْ إِنَّ الْأَمْرَ كُلَّهُ لِلَّهِ ۗ {154}
Ni wake Yeye ufalme wa mbingu na ardhi. Kisha mtarejeshwa kwake.
Mfano wake ni
وَلِلَّهِ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۚ {17}
Na anapotajwa Mwenyezi Mungu peke yake nyoyo za wasioiamini Akhera huchafuka. Na wanapotajwa wenginewe asiye kuwa Yeye basi wao hufurahi.
Washirikina walipokuwa wakisikia kauli ya hapana mola ispokuwa Mwenyezi Mungu (Lailaha illa llah) wanakimbia, na wanaposikia kusifiwa masanamu wanafurahi.
Hivi ndivyo walivyo wabatilifu wa zamani na wa sasa. Haiwapumbazi isipokuwa batili wala haiwatishi isipokuwa haki. Kwenye Nahjulbalagha, amesema: “Ambaye inakuwa uzito kwake kuambiwa haki au kuonyeshwa uadilifu, basi kuyatumia mawili hayo inakuwa uzito zaidi.”
قُلِ اللَّهُمَّ فَاطِرَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ عَالِمَ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ أَنْتَ تَحْكُمُ بَيْنَ عِبَادِكَ فِي مَا كَانُوا فِيهِ يَخْتَلِفُونَ {46}
وَلَوْ أَنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا مَا فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا وَمِثْلَهُ مَعَهُ لَافْتَدَوْا بِهِ مِنْ سُوءِ الْعَذَابِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۚ وَبَدَا لَهُمْ مِنَ اللَّهِ مَا لَمْ يَكُونُوا يَحْتَسِبُونَ {47}
وَبَدَا لَهُمْ سَيِّئَاتُ مَا كَسَبُوا وَحَاقَ بِهِمْ مَا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ {48}
فَإِذَا مَسَّ الْإِنْسَانَ ضُرٌّ دَعَانَا ثُمَّ إِذَا خَوَّلْنَاهُ نِعْمَةً مِنَّا قَالَ إِنَّمَا أُوتِيتُهُ عَلَىٰ عِلْمٍ ۚ بَلْ هِيَ فِتْنَةٌ وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ {49}
قَدْ قَالَهَا الَّذِينَ مِنْ قَبْلِهِمْ فَمَا أَغْنَىٰ عَنْهُمْ مَا كَانُوا يَكْسِبُونَ {50}
فَأَصَابَهُمْ سَيِّئَاتُ مَا كَسَبُوا ۚ وَالَّذِينَ ظَلَمُوا مِنْ هَٰؤُلَاءِ سَيُصِيبُهُمْ سَيِّئَاتُ مَا كَسَبُوا وَمَا هُمْ بِمُعْجِزِينَ {51}
أَوَلَمْ يَعْلَمُوا أَنَّ اللَّهَ يَبْسُطُ الرِّزْقَ لِمَنْ يَشَاءُ وَيَقْدِرُ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ {52}